Friday 27 June 2014

MUHTASARI WA TAARIFA YA MAENDELEO YA WILAYA YA MUHEZA KWA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA MHESHIMIWA DK. JAKAYA MRISHO KIKWETE


Raisi wa Jamuhuri ya Muungano waTanzania   Mhe. Dkt, Jakaya Mrisho Kikwete


MUHTASARI WA TAARIFA YA MAENDELEO YA WILAYA YA MUHEZA KWA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA MHESHIMIWA DK. JAKAYA MRISHO KIKWETE, WAKATI WA ZIARA YAKE
WILAYANI MUHEZA TAREHE 26 MACHI, 2014
Mheshimiwa Rais,
Kwa niaba ya viongozi wenzangu na wananchi wa Wilaya ya Muheza, napenda nitumie nafasi hii kukukaribisha wewe pamoja na ujumbe wako. Tunafuraha kubwa kwa kuwa leo hii upo pamoja nasi hapa Wilayani kwetu kwani wananchi na viongozi wamekuwa na hamu kubwa ya kukuona na kuzungumza nawe.   Karibuni sana.

1.0     UTANGULIZI
Mheshimuwa Rais,
Wilaya ya Muheza ilianza mwaka 1974, ambapo ilimegwa kutoka katika Wilaya ya Tanga. Wilaya ina ukubwa wa kilomita za mraba 1974 kati ya hizo 1,145 zinafaa kwa kwa shughuli za Kilimo na ufugaji.
Wilaya ina Tarafa 4, Kata 33, Vijiji 135 na Vitongoji 522. Wilaya ina Jimbo moja la uchanguzi na Madiwani 44 ambao wote ni kutoka Chama Tawala. Vilevile Wilaya yetu ina Mamlaka ya Mji Mdogo wa Muheza, mamlaka hii inaundwa na  jumla ya Kata 6.
Kwa matokeo ya sensa ya watu na makazi ya mwaka 2012, Wilaya ya Muheza ina wakazi wapatao 204,461 kati yao wanaume ni 100,843 (49.3%) na wanawake ni 103,618 (50.7%) na kiwango cha ongeeko ni 1.4%. Idadi ya kaya zilizopo 47,920 zenye wastani wa wakazi 4.3 kwa kaya.
 
2.0     HALI YA KIUCHUMI
2.1  HALI YA KIPATO KWA MWANANCHI
Mheshimiwa Rais,
Asilimia 90 ya wakazi  hujishughulisha na  shughuli za kilimo. Kipato cha mkazi wa Muheza kwa sasa ni wastani wa Tsh 1,026,000 kwa mwaka na lengo ni kufikia wastani wa Tsh 1,500,000 kwa mwaka ifikapo mwaka 2015. Pamoja na shughuli za kilimo wakazi wa Muheza hujishughulisha na biashara, viwanda vidogovidogo vya useremala, uashi na uhunzi.

2.2   HALI YA MAPATO YA HALMASHAURI
2.2.1 Mapato ya Ndani bila ya fidia ya vyanzo vilivyofutwa
Ukusanyaji wa mapato ya ndani bila fidia ya vyanzo vilivyofutwa umekuwa ukiongezeka kila mwa kutoka Tsh. 590,479,812 (2009/10) hadi  Tsh. 803,818,862 mwaka 2012/2013, kama inavyoonekana hapa chini;
Mwaka
Makisio (Tsh.)
Makusanyo (Tsh.)
% ya makusanyo
2009/10
284,072,000
590,479,812
207.86
2010/11
530,450,000
491,908,462
92.73
2011/12
645,600,000
705,963,718
109.35
2012/13
591,704,000
803,818,862
135.85
2013/14 hadi Desemba
702,691,000
435,626,297
61.99

2.2.2 Mapato ya Ndani pamoja na fidia ya vyanzo vilivyofutwa
Mwaka
Makisio (Tsh.)
Makusanyo (Tsh.)
% ya mapokezi
2009/10
803,142,000
947,022,362
117.91
2010/11
892,435,000
691,373,054
77.47
2011/12
986,836,000
821,509,964
83.25
2012/13
955,940,000
1,164,934,499
121.86
2013/14 hadi Desemba
1,015,127,000
500,736,639.79
49.33


2.2.3 Ruzuku
Mwaka
Makisio (Tsh.)
Makusanyo (Tsh.)
% ya mapokezi
2009/10
10,081,278,117
8,018,144,664
79.54
2010/11
9,951,167,000
10,705,601,164
107.58
2011/12
13,449,077,000
13,481,290,709
100.24
2012/13
15,225,199,540
15,637,807,089
102.71
2013/14 hadi Desemba
25,093,141,910
8,167,904,698.52
32.55

3.0  ILANI YA UCHAGUZI YA CCM YA MWAKA 2010  
Mheshimiwa  Rais ,
Wilaya yetu imeendelea kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya Mwaka 2010 ambayo kwa mujibu wa ibara  21 inalenga kuongeza kasi  ya ukuzaji wa Uchumi wa Kisasa na taifa linalojitegemea kwa kuwashirikisha na kuwawezesha kiuchumi wananchi .
Katika Ilani ya CCM, 2010 zimo ahadi zinazohusu Wilaya ya Muheza, pia wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa Oktoba, 2010, Mhe. Rais, alitoa ahadi mbalimbali ambazo zimeendelea kutekelezwa katika ngazi ya Kitaifa na Kiwilaya. Hali ya utekelezaji wa ahadi hizo imeelezwa kwenye Jedwali Na. 1.
Jedwali Na 1: Utekelezaji wa Ahadi na Maagizo ya Mh. Rais
Na
Ahadi
Utekelezaji
1
Kutatua tatizo la maji Muheza kwa kutekeleza mradi mkubwa utakaotoa maji kutoka mto Zigi.
Usanifu wa Mradi huu ulifanyika mwaka 2011 na Kampuni ya  Arab Consulting Engineers ya Misri na gharama za mradi huu ni zilikadiriwa kuwa Tsh.13.4 billioni.
Hatua zilizochukuliwa na Serikali Kuu
(i)Uendelezaji wa Kisima kirefu cha Polisi kwa kujenga Miundo mbinu ya kusambaza Maji   ambapo kiasi cha Shs 100,000,000 zilizotokana na Ahadi yako Mhe Rais zilipokelewa na kufanyiwa kazi iliyokusudiwa na huduma ya maji inanufaisha wakazi wapatao 900 wa Kata ya Genge.
Hatua zilizochukuliwa na Halmashauri
(ii) Ujenzi wa miundombinu ya maji na uchimbaji wa visima tisa ambapo jumla ya Shs Tsh 363,461,825.28  zimetumika  (Tsh. 229,000,000/= za mapato ya ndani na 134,461,825.28 kutoka Serikali Kuu
(iii)Ununuzi wa mtambo wa kuchimba visima ulioagizwa toka Thailand ambapo jumla ya Shs. 249,140,622.54             zilizotokana na mapato ya ndani zimetumika
(iv) Maandiko  ya kutafuata fedha yameandaliwa na kuwasilishwa kwa Taasisi za ENCODIA ya Ugiriki, ACE Consulting Engineer – Moharram- Bakoum     na EUROHNSA S.A- Madrid                      
2
Kutatua matatizo ya  uhaba wa ardhi Muheza kwa kufuta hati za mashamba ya Mkonge yaliyotelekezwa muda mrefu kwa kufuata taratibu za kisheria.
Halmashauri imewasilisha maombi kwa  Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi ya kubatilisha hati za umiliki wa ardhi wa mashamba nane ambapo asilimia kubwa ya mashamba  haya yamevamiwa na Wananchi Maombi haya yaliwasilishwa kwa nyakati tofauti( 2007,2009,2010 & 2012 )  .Mpaka sasa Halmashauri inaendelea kusubiri utekelezaji wa maombi hayo hata hivyo mashamba haya yamevamiwa na Wananchi . Uongozi wa Mkoa na Wilaya katika kuhakikisha wananchi wa Derema waliopisha Hifadhi ya Msitu wa Amani wanapata fidia yao ya Ardhi Mbadala waliyoahidiwa miaka kumi iliyopita ilikutana na Wadau wa Shamba la Kibaranga  na makubaliano yamefikiwa kuwa Shamba la Mkonge Kibaranga lipimwe na kugawiwa kwa wahanga hao wa Derema, wakulima wakubwa na wakati wa zao la Mkonge  pamoja wananchi wenye uhitaji . Hadi sasa ekari 1224 (mashamba 408) zimepimwa. Taarifa maalumu ya shamba la kibaranga imeambatanishwa.
3
Ujenzi wa barabara ya lami kutoka Muheza hadi  Amani

Matengenezo ya mara kwa mara yamekuwa yakifanyika hasa sehemu zilizokuwa korofi, hali inazidi kuimarika.  Barabara hiyo ilimetengewa fedha mwaka 2013/2014 kwa ajili ya upembuzi yakinifu na fedha zimetolewa   kazi ya upembuzi yakinifu inaendelea.
4
Ujenzi wa bwalo shule ya Sekondari Muheza High School ahadi ambayo uliitoa wakati wa kufungua shule hii tarehe 19/7/2008
Ahadi hii mpaka sasa haijatekelezwa.
5
Ununuzi wa gari la wagonjwa (ambulance) kwa ajili ya hospitali Teule Muheza
Maombi maalumu ya fedha za utekelezaji wa ahadi hii yamewasilishwa Wizara ya Fedha (Hazina) wakati wa bajeti ya mwaka 2011/12 na Wilaya imeendelea kukumbusha kila mwaka, pia katika bajeti ya mwaka 2014/2015 maombi maalumu yamewasilishwa tena Hazina. Mpaka sasa Ahadi hii haijatekelezwa.


MAAGIZO
1
Kujenga maabara katika shule za Sekondari

Hadi sasa Halmashauri ya wilaya ina vyumba vya maabara 8 kwa masomo ya sayansi kati ya 75 zinazohitajika,
meza za maabara (mobile laboratory) 6 na madarasa ya  sayansi 17 (Vyumba vya sayansi) kwa shule za Serikali, ujenzi wa maabara 67 katika shule zote za serikali upo katika hatua mbalimbali  kwa kutumia fedha za Serikali na nguvu za Wananchi.
·         7 hatua umaliziaji.
·         2 hatua ya Lenta.
·         5 Ujenzi wa Boma
·         8 hatua ya kumwaga jamvi.
·         16 msingi umekamilika
·         20 hatua ujenzi wa msingi
·         5 Maandalizi ya awali
·         6 utekelezaji haujaanza
 Lengo ni kuhakikisha kuwa Shule zote za Serikali zinakuwa na maabara tatu kwa masomo ya sayansi hadi Novemba mwaka 2014.

4.0 MIPANGO YA MAENDELEO YA WILAYA
Wilaya ya Muheza kwa kushirikiana na sekta Binafsi, Vyama vya Siasa, Wadau wa Maendeleo na Wananchi inatekeleza Mipango mbalimbali ya Kitaifa ikiwemo;
·         Malengo ya Maendeleo ya Millenia (MDGs)
·         Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010
·         Mpango wa Uwiano wa Maendeleo wa  Miaka 5 wa Wilaya (DIDP) kuanzia mwaka 2011/12 hadi 2015/2016.
·         Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (BRN)



UTEKELEZAJI WA MPANGO WA TEKELEZA SASA KWA MATOKEO MAKUBWA KWA MIAKA YA 2013/2014- 2014/2015 (BRN)
Pamoja na vipaumbele vya kitaifa katika mpango huu, Wilaya imejiwekea vipaumbele vyake ambavyo ni;
a)      Kukuza mapato kwa mtu mmoja mmoja kutoka wastani wa Tsh. 1,026,000 kufikia wastani wa Tsh. 1,500,000 mwaka 2015 na Mamlaka za Serikali za Mitaa kutoka wastani wa makusanyo ya 4% hadi 15% ya bajeti ifikapo mwaka 2015).

Mafanikio
·         Miradi ya kuongeza kipato kwa wananchi yenye thamani ya Tsh. 2,369,027,016/= imetekelezwa ikiwemo; ujenzi wa masoko 2, boreshaji wa kilimo cha zao la michungwa na mahindi, ngombe bora 40 wamegawiwa kwa wananchi, vituo vya kukusanya maziwa 2 vimejengwa na mizinga ya nyuki 170 ya kisasa imesambazwa, pia mikopo ya makundi maalumu (kinamama na vijana) ya Tsh. 70,000,000/= imetolewa.
·         Ukusanyaji mapato umeongezeka toka Tsh. 590,479,812/= (2009/10) hadi  Tsh. 803,818,862/= (2012/13)
b)      Sekta ya Kilimo:  Lengo ni kuongeza uzalishaji wa zao la mahindi na machungwa kwa Kuongeza uzalishaji wa mahindi kutoka tani 1.8 hadi tani 2.0/ha ifikapo Julai 2014 na kuongeza uzalishaji wa machungwa kutoka tani 10 hadi tani 12 ifikapo Julai 2015
Utekezaji kufikia malengo
·         Matumizi ya matrekta makubwa yameongezeka kutoka 70 mwaka 2012 hadi  73 mwaka 2013 na matrekta madogo  ya mkono toka toka 45 mwaka 2012 hadi 55 mwaka 2013
·         Uzalishaji wa mazao ya chakula umeongezeka toka tani 106,593 kwa mwaka 2012 hadi tani 142,149 kwa mwaka 2013
·         Juhudi kuogeza uzalishaji wa zao la michungwa, lita 400 za sumu ya kudhibiti inzi waharibifu wa machungwa zimenunuliwa na 180 zimesambazwa kwa wakulima mwaka 2013
·         Wilaya inaendeleza Skimu za umwagiliaji za  Misozwe, Mashewa, na Potwe ipo katika hatua za upembuzi yakinifu.  Kupitia Skimu hizo wilaya inategemea kuongeza uzalishaji wa Mahindi na Mchele  kwa tani 2,460.

c)      Sekta ya Mifugo:             Lengo ni kuongeza uzalishaji wa maziwa ya ng’ombe kutoka wastani wa lita 6  hadi 10 kwa ngombe kwa siku hadi ifikapo 2015

·         Utekelezaji kufikia malengo
·         Mitamba ya ngombe 40 imenunuliwa na kusambazwa kwa wafugaji 40 katika Tarafa za Amani na Muheza mwaka 2013
·         Uzalishaji maziwa umeongezeka toka lita 5,525,075 mwaka 2011 hadi lita 6,456,550 kwa mwaka 2013
·         Majosho 2 ya kuogeshea ng’ombe ya Kigombe na Muungano yamekarabatiwa na yanafanya kazi
d)     Sekta ya Mazingira: Lengo kuongeza uzalishaji wa mazao ya nyuki hapa wilayani
·      Asali kutoka  kilo 400  na kilo 5,000  ifikapo Juni 2015
·      Nta kutoka kilo 20 hadi kilo 300 ifikapo mwaka 2015

Utekelezaji kufikia malengo
·         Mizinga ya nyuki 170 ya kisasa na 60 ya kienyeji  imetengenezwa katika Tarafa za Amani na      Bwembwera
·         Vijiji 15 vimeanzisha hifadhi ya misitu ya asili ambapo shughuli za utunzaji wa mazingira kampeni za upandaji miti na uthibiti wa moto zinafanyika ambapo miche 2,300,120 imepandwa mwaka 2012 na 1,516,198 imepandwa 2013.
·         Upandaji miti misitu ya asili ya vijiji

e)      Sekta ya Elimu
Elimu Msingi Lengo ni:
·         Kuinua kiwango cha ufaulu katika Mtihani wa darasa la VII kutoka  (27%) (2012) hadi kufikia  65% (2013).
·         Kuinua kiwango cha ufaulu katika Mtihani wa Darasa la IV kutoka 90% (2012) hadi (95%) mwaka 2013.
·         Kuwa na asilimia 100 ya wanafunzi wa darasa II – VII wanaojua Kusoma, Kuandika na Kuhesabu (KKK).  
Utekezaji kufikia malengo
·         Wilaya imehakikisha kila shule inakuwa na Kiongozi cha Usimamizi wa shule, miundombinu muhimu ya shule imeboreshwa, Ruzuku za uendeshaji wa shule zimetolewa, Kuandikisha wanafunzi 6,000 wa darasa la kwanza, Kupunguza Mdondoko na utoro, kuhimiza chakula cha mchana mashuleni.
·      Darasa la saba ufaulu umeongezeka toka 27% (2012) hadi 66 (2013) na mtihani wa darasa la IV ufaulu umeongezeka toka 90% (2012) hadi 96% (2013)
·         Matokeo ya mitihani yameongezeka kwa shule zinazoingia katika kundi la ‘Green’  kutoka shule 52 (46%) katika Mock Mkoa hadi 70 (63%) katika PSLE ongezeko la shule  18 sawa na 17%.
·         Mimba kwa wanafunzi zimepungua kutoka 4 mwaka 2012 hadi 2 mwaka 2013
·         Asilimia ya wanafunzi wa darasa II – VII wanaojua Kusoma, Kuandika na Kuhesabu (KKK) imeongezeka toka 90% mwaka 2013 hadi 92% mwezi Machi 2014.

Elimu Sekondari malengo yaliyowekwa ni:
·         Kuongeza kiwango cha ufaulu wa wanafunzi katika mtihani wa kidato cha pili kutoka 32% ya mwaka 2012 hadi kufikia  86% ifikapo mwaka 2015.
·         Kuongeza kiwango cha ufaulu wa wanafunzi wa kidato cha Nne kutoka 19%  ya mwaka 2012 hadi 65% ifikapo mwaka 2015
·         Kuongeza kiwango cha ufaulu wa wanafunzi wa kidato cha sita kutoka 86% ya mwaka 2012 hadi kufikia 100%  ifikapo mwaka 2015

Utekelezaji kufikia malengo –
  • Ili kufikia malengo Wilaya imeteua walimu wakuu kwa kila shule kwa shule zilizokuwa na Kaimu wa Wakuu wa shule
  • Kuimarisha usimamizi wa shule kwa kuhakikisha kila shule ina Bodi ya Shule yenye wajumbe wenye sifa na iliyo hai
  • Kufanya vikao na walimu ili kufahamu matatizo yao
  • Kufuatilia kwa karibu matumizi sahihi ya fedha za  Ruzuku ya ‘Capitation’
  • Kuhimiza na kusimamia mitihani yote ya ndani.
·      Ufaulu kidato cha pili umeongezeka toka 32% (2012) hadi 49% (2013)
·      Ufaulu kidato cha nne umeongezeka toka 19% (2012) hadi 36% (2013)
·      Ufaulu kidato cha sita umeongezeka kutoka 86% mwaka 2012 hadi 89% mwaka 2013
·         Matokeo ya mtihani wa kidato cha Nne (Upangaji wa wanafunzi kwa madaraja)
-          Kijani imeongezeka kutoka 11 hadi 34
-                Njano imeongezeka kutoka 470 hadi 904
-                Nyekundu imepungua kutoka 1,745 hadi 267

f)       Sekta ya Afya
Lengo ni kuongeza idadi ya wanachama wanaojiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF) kutoka  wastani wa sasa wa 17%  hadi 50% ifikapo 2015
Utekelezaji Kufikia malengo.
·            Kaya zilizojiunga na mfuko wa CHF zimeongezeka toka 1,860 mwaka 2012 hadi 7,730
        mwaka 2014, kati yake Wazee ni wakiwa 4,678. Tumefikia lengo kwa asilimia 34% ya
 kaya zote 22,698 zilizolengwa
·            Idadi ya vituo vya kutolea huduma imeongezeka kutoka 43 mwaka 2012 hadi 47 mwaka
        2014.
·            Ujenzi wa majengo ya wagonjwa wa nje (OPD) katika vituo vya afya vya Mhamba na
Misalai umekamilika na huduma za afya zinatolewa
·            Vifaa tiba vya thamani ya sh.74,338,600 vimenunuliwa pamoja na dawa kiasi cha kutosha
         zimeagizwa kwa mfumo wa kuagiza dawa kulingana na mahitaji halisi ya kituo husika
         (Integrated Logistic System – ILS).

g)      Sekta ya Maji
Malengo ya Mwaka 2013/2014
·         Kuhakisha kwamba vijiji 7 kati ya 10 vya program vinapata maji safi na salama
·         Kujenga vituo 66 vya kuchotea maji (DP)
·         Watu wapatao 39,905 wanapata huduma ya maji kwa umbali usiozidi mita 400



Utekelezaji kufikia malengo
·         Miradi 4 ambayo inahudumia vijiji 6 vya Ubembe, Kisiwani Nkumba,  Kibanda Nkumba, Kwemhosi, Mamboleo na Masimbani imekamilika na vituo 40 vimejengwa ambapo watu wapatao  6,902 wanapata huduma ya Maji. Aidha miradi 3 iko katika hatua mbalimbali, vijiji vya Misongeni na Mikwamba (inakamilika Aprili), na Kigongomawe (unakamilika Mei) ambapo jumla ya watu 4,247 watapata huduma ya maji.
·         Upatikanaji maji vijijini umeongezeka toka 56.3% mwaka 2011 hadi 62.2% mwaka 2013
·         Miundombinu ya uvunaji wa maji ya mvua imejengwa katika shule za msingi 11, Sekondari 5 na Zahanati 8. Aidha jumla ya miradi 6 ya programu ya maji vijijini inayoendelea kujengwa ina kipengele cha ujenzi wa miundombinu ya uvunaji wa maji ya mvua katika taasisi za kijamii.

h)     Usimamizi na ufuatiliaji
Kamati ya Usimamizi inayongozwa na Mkuu wa wilaya
  • Mkuu wa Wilaya – Mwenyekiti
  • Katibu Tawala (W) – Mjumbe
  • Afisa Usalama (W) – Mjumbe
  • Mwenyekiti wa Halmashauri- Mjumbe
  • Mkurugenzi Mtendaji Wilaya – Katibu
  • Afisa Mipango (W) - Mjumbe

Kamati ya DDU
·                  Imeundwa ina wajumbe 3 na inafanya kazi
·         Inawajibika kwa Mkurugenzi Mtendaji (W).
Mfumo wa ufuatiliaji
  • Ukaguzi -Mkurugenzi, Madiwani, Timu ya Ufuatiliaji, DDU
  • Ufuatiliaji - Mkurugenzi, Madiwani, Wakuu wa Idara, Timu ya Ufuatiliaji, DDU
  • Vikao - Mkurugenzi, Timu ya Ufuatiliaji, Madiwani



5.0 SEKTA YA UZALISHAJI - (SURA YA TATU YA ILANI YA CCM MWAKA 2010)
5.1 SEKTA YA KILIMO
5.1.1 Mazao yanayolimwa
Mazao ya biashara yanayolimwa ni Machungwa, Chai ambayo hulimwa na makampuni yanayomiliki mashamba makubwa  (Estates) na wakulima wadogowadogo , mazao ya viungo (Iliki, karafuu, Mdalasini, Pilipili manga), Miwa, Minazi, Katani, Korosho na mazao ya chakula ni pamoja na Mahindi, Mihogo, Ndizi,  maharage, Mpunga na viazi vitamu.
5.1.2 Hali ya chakula.
Katika kipindi cha mwezi Februari hali ya chakula iliendelea kuwa ya kuridhisha katika maeneo yote ya Wilaya kutokana na kuwepo kwa vyakula vya wanga kama mihogo na ndizi vya kutosheleza mahitaji na ziada. Vyakula vilivyopo ni pamoja na Mahindi, Mpunga, Viazi vitamu, mikunde, ndizi na mihogo iliyozalishwa msimu wa masika na vuli 2013.
Hadi mwishoni mwa mwezi Februari, 2014 Wilaya ilikuwa ina akiba ya chakula cha wanga kiasi cha tani    70,392 za mahindi na mpunga/mchele ulioko ghalani kwa wakulima na wafanyabiashara na muhogo pamoja na ndizi vinavyovunwa shambani. Mahitaji ya chakula kwa Wananchi wa Muheza ni tani 48,509 hivyo Wilaya ina ziada ya tani 21,883 ya chakula.
Mchanganuo wa chakula kilichopo ghalani na mashambani ni kama ifuatavyo;
Na
Aina ya zao
Kiasi (Tani)
1
Mahindi
13,269
2
Muhogo
42,398
3
Ndizi
14,321
4
Mchele
404

Jumla
70,392
5.1.3 Uzalishaji wa mazao ya chakula
S/N
ZAO
MWAKA 2011 (TANI)
MWAKA 2012 (TANI)
MWAKA 2013 (TANI)
1.
Mahindi
35,979
20,117
29,853
2.
Muhogo
54,283
50,307
55,436
3.
Ndizi
57,770
34,656
52,029
4.
Mpunga
5,383
807
2,922
1.       
Mikunde
2,230
706
1,909

Jumla
155,645
106,593
142,149
·         Mwaka 2012 uzalishaji ulishuka kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa.
·         Uzalishaji wa mahindi umeongezeka toka tani 1,8 kwa hekta hadi 2.5 kwa hekta
5.1.4 Uzalishaji wa mazao ya biashara
S/N
ZAO
MWAKA 2011 (TANI)
MWAKA 2012 (TANI)
MWAKA 2013 (TANI)
1
Machungwa
79,830
79,930
80,430
2
Mazao ya viungo
2,760
2,903
3123
3
Nazi
183,590
183,670
183,715

JUMLA
266,180
266,503
267,268

5.1.5 Mkakati wa kuongeza kipato cha mwananchi kupitia zao la michungwa
Katika kuongeza uzalishaji wa zao la Machungwa ambalo ndio zao la mnyororo wa thamani kwa  Wilaya yetu,  hatua zifuatazo zimechukuliwa;-
·         Mashamba darasa 12 yameanzishwa katika maeneo ya Mamboleo, Kwakibuyu, Songa Kibaoni, Magoda, Mkuzi, Kilulu, Mtindiro, Mkinga, Mpakani, Mkwakwani na Kwakifua
·         Kuendeleza vitalu vya miche bora ya machungwa ikiwemo aina ya machungwa isiyo na mbegu (seedless) vilivyoko Maduma, Kilongo na Songa. Uzalishaji wa miche ni kama ifuatavyo;
-          2011/12           -           miche 5,000
-          2012/13           -           miche 9,000
-          2013/14           -           miche 15,000
·         Kununua dawa ya kuua inzi wa machungwa na kuuza kwa bei nafuu kupitia vyama vya wakulima wa machungwa kwa bei ya Tsh. 22,700/= kwa lita badala ya 27,000 – 30,000/= katika maduka ya pembejeo hadi sasa lita 400 zimenunuliwa na 180 zimeuzwa.
·         Kupambana na inzi wa machungwa kwa kuweka siku maalumu kila mwezi ya kufukia machungwa ili kuangamiza mazalia ya inzi.
·         Kujenga kituo cha kuongeza thamani ya machungwa kwa kuyapanga kwa madaraja, kufungasha na kuhifadhi kwenye chumba cha baridi, Tsh. 74 milioni zimetengwa kwa kazi hiyo.
·         Halmashauri ya Wilaya kwa kushirikiana na Mradi wa Muungano wa Ujasiriamali Vijijini (MUVI) wametoa mafunzo ya kilimo cha kibiashara katika zao la machungwa kwa wakulima 1400 Maafisa Ugani 45.
·         Vyama vya Akiba na Mikopo (SACCOS) 4 vimeanzishwa na kuendelezwa katika maeneo yanayolima machungwa (Kata za Songa, Kilulu, Nkumba na Mtindiro ili kuwezesha wakulima kupata mikopo yenye riba nafuu na uhamasishaji wa uundaji wa vyama vingine zaidi umefanyika katika kata  za Kwafungo na Tingeni.

5.1.5 Mkakati wa kuongeza kipato cha mwananchi kupitia mazao ya viungo (iliki, mdalasini, karafuu na chai)
·         Kumekuwepo na ongezeko la uzalishaji wa mazao ya viungo kila mwaka ambapo tani 2, 760 zimezalishwa mwaka 2010/11, tani 2,903 mwaka 2011/12 na tani 3,123 mwaka 2012/13, hii inatokana na bei nzuri iliyopo hivyo kuongeza upandaji wa mazao haya
·         Wilaya kushirikiana na Jumuia ya Wakulima wa Kilimo Hai Usambara Mashariki (JUWAKIHUMA) wametoa mafunzo ya utunzaji wa vitalu katika vijiji 7 na wakulima 720 wamepatiwa elimu ya kilimo bora cha viungo
·         Wakulima wa mazao ya viungo wamefanya vikao 2 kujadili kutovuna mazao kabla ya kukomaa ili kupata soko la uhakika na bei nzuri, mikutano hiyo imewezesha pilipilimanga kuuzwa kwa bei ya Tsh. 8,500/= kwa kilo badala ya Tsh. 6,500/=
·         Chama cha kuweka na kukopa (SACCOs) kimeanzishwa katika kata ya Nkumba ili wakulima waweze  kupata mikopo yenye riba nafuu na kuondokana na kuuza mazao kabla ya kukomaa.
·         Wakulima wa mazao ya viungo wamehamasishwa kuanzisha ushirika wa wakulima, ambapo taratibu za uanzishaji zinaendelea.
5.1.6 Mkakati wa kuongeza kipato cha mwananchi na pato la Halmashauri ya wilaya kwa mazao mapya
Zao la Korosho  ni miongoni mwa mazao ya biashara ambayo Wilaya imeanza kuyapa kipaumbele, ambapo kuanzia mwaka  2013/14 mfumo wa stakabadhi ghalani na kuuza korosho kwa njia ya mnada na kuanzisha mashamba darasa umeanzishwa  na  jumla ya hekta 99 zimelimwa. Mwaka 2013/2014 korosho zimeuzwa kati ya Tshs. 1,250/=  na Tshs1,360/= kwa kilo ya daraja la kwanza na Tshs 900 kwa kilo kwa daraja la pili na jumla tani 4 zimeuzwa kwa utaratibu wa kukusanya na kuuza kwa pamoja bila kutegemea mkopo toka taasisis za fedha, uvunaji unaendelea, mafanikio machache yameanza kujitokeza ambapo;
·         Uzalishaji umeongezeka kutoka tani 10 mwaka 2010 /2011 hadi tani 25 mwaka 2012/2013.
·         Miche bora ya korosho 850 imesambazwa na kupandwa kwa wakulima mwaka 2012/2013. Mashamba darasa 20 yameanzishwa na kuendelezwa kwa kushirikiana na Bodi ya korosho na madawa ya ruzuku yamesambazwa kwa wakulima.
·         Elimu ya kilimo bora cha korosho imetolewa kwa wakulima 300 na wabanguaji 26.
Wilaya kwa kushirikiana na Bodi ya Korosho husambaza mbegu na miche bora ya Korosho, kujengea uwezo Chama cha wakulima wa Korosho Ngomeni

5.1.7 Upatikanaji na matumizi ya zana za kilimo
Wilaya imeweka juhudi katika kuongeza upatikanaji na matumizi ya zana za kilimo kwa kuishirikisha sekta binafsi, kuhamasisha na kuwezesha vikundi vya wakulima katika matumizi ya zana bora za kilimo hususan kwa vijana kupata mikopo ya pembejeo na zana za kilimo kutoka kwenye mfuko wa pembejeo.

5.1.8 Matumizi ya mbegu bora
Wilaya imefanya juhudi mbalimbali ili kuboresha uzalishaji wa Mazao. Miongoni mwa juhudi hizo ni pamoja na;
  • Uzalishaji wa mbegu za Mahindi zilizothibitishwa (CS – Certified Seeds) ambapo tani 110 zimezalishwa msimu wa 2012/2013



Uzalishaji wa mbegu bora
Mwaka
Mahindi ya mbegu
Mahindi ya lishe
2010
Tani 23.9
Tani 12
2011
Tani 64
Tani 40
2012
Tani 1
Tani 0
2013
Tani 60
Tani 50

  • Kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha kilimo cha Sokoine (SUA) wakulima wa kijiji cha Tongwe wamewawezesha kuwa na kituo chenye mashine ya kusindika muhogo. Kituo hiki kina uwezo wa kuzalisha tani moja kwa wiki.
5.1.9 Mapokezi ya Vocha za Pembejeo za Ruzuku
Wilaya ya Muheza ni miongoni mwa Wilaya zinazopata pembejeo za ruzuku katika Mkoa wa Tanga. Matumizi ya pembejeo za Ruzuku yameongezeka toka 34% mwaka 2010/11 hadi 100% mwaka 2012/13 kwa pembejeo za Ruzuku zilizoletwa hapa Wilayani.
Mgao wa pembejeo za ruzuku kwa kipindi cha miaka 3 ulikuwa kama ifuatavyo:-
MWAKA
2010/2011
2011/2012
2012/2013
2013/2014
IDADI YA VOCHA
30,000
16,800
18,000
14,400

5.1.10 Matumizi ya Trekta
Vikundi 27 pamoja na wamiliki binafsi 13 wa matrekta wamehamasika kutumia matrekta madogo ili kupanua wigo wa eneo la matumizi ya kilimo na kuongeza uzalishaji. Vikundi na watu binafsi wamehamasishwa na kuunganishwa na SUMA JKT kwa ajili ya kupata mikopo ya matrekta, kikundi kimoja na watu binafsi 28 wamejaza fomu wanangoja kufanyiwa tathmini na SUMA J.K.T. Aidha trekta kubwa moja na power tiller 10 zimenunuliwa na watu binafsi. Pia Vikundi 25 vyenye wanyama kazi wamepatiwa elimu ya matumizi bora ya wanyamakazi.

Hadi sasa Wilayani kuna jumla ya matrekta 73 kati ya hayo matrekta 62 yanafanya kazi na 11 yanahitaji matengenezo.

Matumizi ya matrekta makubwa yameongezeka kutoka 57 mwaka 2010 hadi 73 mwaka 2013
MWAKA
2010
2011
2012
2013
2014 (hadi Februari)
Matrekta makubwa
57
57
70
73
73
Matrekta ya mkono
43
43
45
53
55
JUMLA
100
100
115
126
128


5.1.11 Umwagiliaji
Ibara ya 19 ya ilani ya Chama Chama Tawala inalenga Kujenga Misingi ya Uchumi wa Kisasa wa taifa linalojitegemea. Ili kuongeza uzalishaji na kuondokana na kilimo cha kutegemea mvua wananchi wamehamasishwa juu ya kilimo cha umwagiliaji na uboreshaji wa miundombinu unaendelea ambapo Skimu za umwagiliaji za Misozwe, Mashewa zinaendelezwa na ya Potwe ipo katika hatua za upembuzi yakinifu ili kubaini maeneo yanayofaa kwa kilimo cha umwagiliaji. Skimu hizi zitakapokamilika zitakuwa na uwezo wa kumwagilia hekta 250 (Misozwe 100, Mshewa 50 na Potwe 100). Kupitia Skimu hizo wilaya inategemea kuongeza uzalishaji wa Mahindi na Mchele kwa tani 2,460. Aidha, Wilaya imenunua pampu rahisi 30 za umwagiliaji na kuzisambaza kwa vikundi vitatu vya wakulima.
Halmashauri ya Wilaya imetekeleza jumla ya miradi kumi ya kilimo kwa mwaka 2011/12 hadi 2012/13 yenye thamani ya Ths.1,920,636,494.00.

5.2 SEKTA YA MIFUGO
Ibara ya 38 inasisitiza kuiendeleza Sekta ya Mifugo kwa ari zaidi, nguvu zaidi na kasi zaidi ili kuiwezesha kutoa mchango mkubwa kwenye Pato la Taifa. Hapa Wilayani uendelezaji sekta hii unafanywa kwa ushirikiano na wadau wa mifugo waliopo Wilayani kama vile World visión, Land O’Lakes, Brac Tanzania na vyama vya ushirika vya msingi na ufugaji wa ng’ombe wa maziwa.
Jumla ya wafugaji 420 wamepatiwa elimu ya ufugaji wa kibiashara na 320 wamepata mafunzo juu ya matumizi ya majosho yanayozingatia uhifadhi wa mazingira, pia miundombinu ya mifugo imeboreshwa ikiwemo majosho 2, mnada1, mabwawa 2 na machinjio 1.
5.2.1 Idadi ya Mifugo na uzalishaji wake
Katika wilaya ya Muheza kuna mifugo 380,854 kati ya hiyo ng’ombe ni 28,747 (chotara 9,915 na asili 18,832), Mbuzi 45,483 (chotara 1,007, asili 44,476), Kondoo 5,457, Nguruwe 2,040, Punda 227 na kuku wa asili 294,229 na kuku wa mayai 4,671.
5.2.2 Uzalishaji wa maziwa
MWAKA
2010/2011
2011/2012
2012/2013
Uzalishaji kwa lita
5,525,075
6,029,030
6,456,550

5.2.3 Uzalishaji wa Nyama
MWAKA
NG’OMBE (Kg)
MBUZI (Kg)
KONDOO (Kg)
NGURUWE (Kg)
2010/2011
378,840
67,995
7,988
42,118
2011/2012
397,100
74,190
9,945
43,001
2012/2013
399,103
76,053
10,112
43,781

1,175,043
218,238
28,045
128,900





5.2.4 Uhamilishaji
Huduma ya uhamilishaji inatolewa kupitia vyama vya ushirika wa wafugaji wa ng’ombe wa maziwa (Muheza – CHAWAMU na Amani- UWAMA) pamoja na wadau wa sekta binafsi wakiwemo World vision- Tanzania na Brac Tanzania’ wafugaji hupatiwa huduma hii muhimu kwa njia ya kukopeshwa na baadaye kulipa wakati wa malipo ya mwezi ya mauzo ya maziwa. 
Idadi ya ng’ombe waliohamilishwa na ndama waliozaliwa katika kipindi cha miaka mitatu ni kama ifuatavyo;
Mwaka
Idadi ya ng’ombe waliopandishwa
Idadi ya ndama
Idadi ya ndama jike
Idadi ya ndama dume
2010/11
412
248
123
125
2011/12
439
265
134
131
2012/13
448
269
129
140
Miundombinu sekta ya mifugo imeboreshwa na jumla ya miradi 7 imetekelezwa yenye thamani ya Shilingi 415,265,267.00 katika kipindi cha mwaka 2012/2013 hadi Januari, 2014

5.3 USHIRIKA NA MASOKO
Wilaya ina vyama vya ushirika 37 ikiwemo vyama vya akiba na mikopo 23, Ushirika wa mazao 7 vyenye wanachama 332 na hisa Tsh. 7,224,000/=, vyama vya wafugaji 5 na aina nyingine 2 vyenye wanachama 48 na hisa zenye thamani ya Tsh. 1,380,000/=
5.3.1 Vyama vya akiba na mikopo (SACCOS)
Mwaka
Idadi ya SACCOS
Wanachama
Hisa
Akiba
Amana
Mikopo (000)
Idadi ya vikundi
Me
Ke
Jml



Tolewa
Rejeshwa
2011
22
83
1448
886
2417
126,794,000
785,042,000
44,685,000
3,360,826
1,995,528
2012
22
83
1448
886
2417
126,794,000
796,080,000
46,115,000
3,460,826
2,095,528
2013
23
105
1625
840
2570
130,561,000
805,262,000
62,142,000
3,673,493
2,624,524

5.3.2 Vyama vya wafugaji
Mwaka
Idadi
Wanachama
Hisa
Me
Ke
Jml

2011
3
737
269
1006
9,810,000
2012
3
737
269
1006
9,810,000
2013
5
833
327
1160
13,605,000








5.4 SEKTA YA UVUVI
Uvuvi hapa Wilayani unafanyika katika bahari ya Hindi hasa kwa wakazi wa kata ya Kigombe na kwenye mabwawa ya ufugaji samaki. Kuna mabwawa 6 yaliypandikiwa samaki aina ya sato kwa ajili ya kuzalisha vifaranga katika Kata ya Misozwe.  
Ili kuboresha shughuli za uvuvi Wilayani kwa kipindi cha Januari - Desemba 2012/13 wavuvi na wachuuzi 120 wamepatiwa mafunzo juu ya udhibiti wa ubora wa mazao ya uvuvi ili kukidhi mahitaji ya soko la ndani na nje katika Kata ya Kigombe. Aidha Wilaya imefanya doria shirikishi 12 kati ya hizo doria za baharini 9 na nchi kavu 3 dhidi ya uvuvi haramu.
Aidha Wilaya imetekeleza jumla ya miradi nane ya Sekta ya Mifugo kwa mwaka 2011/12 hadi 2012/13 yenye thamani ya Ths. 448,390,522.00.


5.5 SEKTA YA BARABARA, MAWASILIANO NA UCHUKUZI
Njia kuu ya usafiri zinazotumiwa na Wananchi  Wilayani ni barabara. Aidha mawasiliano ya simu za mkononi yanapatikana, Mitandao inayopatikana Wilayani Muheza ni  Tigo, Airtel, Vodacom na Zantel. Mitandao ya simu imerahisisha huduma za mawasiliano Vijijini na huduma za fedha. Aidha imesaidia kuboresha biashara na masoko ya bidhaa ya mazao ya Kilimo kwani simu zinatumika kuwaunganisha wateja na wakulima.

5.5.1 Barabara
Mtandao wa barabara Wilayani una urefu  wa kilometa 818.2 kati ya hizi kilometa 693 zinasimamiwa na Wilaya na kilometa 125.2 zinasimamiwa na wakala wa barabara Tanzania yaani TANROADS. Kati ya kilomita 818.2 barabara kuu ni km 42, barabara za mkoa km 83.2, barabara za Wilaya /Vijiji km 673.4 na kilomita 19.6 barabara za Mjini.
Mtandao wa barabara zinazopitika kwa kipindi cha mwaka mzima umeongezeka toka kilomita 250 mwaka 2010/11 hadi 393 mwaka 2012/13 kama inavyoonekana kwenye jedwali.

MWAKA
2010/2011
2011/2012
2012/2013
Barabara zinazopitika kwa mwaka mzima.
250
309
393

Aidha vijiji 2 havijaunganishwa na mtandao wa barabara, Pia baadhi ya barabara zinapitika kwa shida kipindi cha msimu wa mvua ikiwemo barabara za Zigi - Kwemdimu, Lunguza - Kambai na Potwe - Kimbo. Wananchi hupata usumbufu wa kufikisha bidhaa  zao sokoni kutokana na hali ya barabara. Wilaya  inaendelea kutekeleza matengenezo ya barabara mbalimbali Wilayani ili kuboresha usafiri na mawasiliano.
Halmashuri ya Wilaya hutumia wastani wa Tsh. 750,000,000/= kwa mwaka katika matengenezo ya barabara, ambazo zimesaidia kuimarika kwa barabara za Wilaya.
Aidha Wilaya imetekeleza jumla ya miradi hamsini na tatu kwa mwaka 2011/12 hadi 2012/13 yenye thamani ya Ths. 968,934,500.00.

5.6  SEKTA ARDHI, MALIASILI NA MAZINGIRA
5.6.1   Sekta ya Ardhi
Wilaya ya Muheza ina jumla ya kilomita za mraba 1974 ambapo zinajumuisha ukanda wa bahari. Eneo linalofaa kwa kilimo ni 85% ya eneo la Wilaya. Hata hivyo sehemu kubwa ya eneo hilo ni sehemu ya mashamba makubwa ya mkonge, mpira na mifugo ambayo yanamilikiwa na watu/mashirika na ambayo hayaendelezwi ipasavyo yenye eneo la hekta 59,795.32. Hii inapelekea kuwepo kwa migogogo mingi ya ardhi. Migogoro hiyo ya ardhi inahusu uvamizi katika mashamba makubwa yaliyotelekezwa.
Pamoja na migogoro ya mashamba pia ipo migogoro ya mipaka ya Wilaya, mgogoro kati ya Serikali na Wananchi, migogoro ya mipaka ya vijiji na migogoro ya viwanja. Maeneo yenye migogoro ni pamoja na mashamba 7 ya Mkonge, shamba la mifugo lililopo Azimio na shamba la mifugo la Mivumoni. 
Aidha kuna mgogoro wa mpaka kati ya Wilaya ya Muheza na Wilaya za Tanga na Pangani. Hatua za kutatua mgogoro uliopo kati ya Wilaya ya Tanga na Muheza unaendelea kushughulikiwa katika ngazi ya Mkoa na ule kati ya Wilaya ya Muheza na Pangani mazungumzo kati ya uongozi wa Wilaya hizo mbili bado yanaendelea ili kufikia muafaka.

5.6.2 Ufumbuzi wa migogoro ya mashamba
Halmashauri ya Wilaya imefanya taratibu za kuomba kubatilishwa kwa miliki za Mashamba yaliyotelekezwa yenye ukubwa wa eneo la hekta 24,627 kwa kufanya mambo yafuatayo:-
·         Kuwasilisha mapendekezo kwenye Baraza la Halmashauri ambalo lilidhiinisha mapendekezo ya kufutwa kwa hatimiliki za Mashamba hayo ili wagawiwe wananchi wenye uhaba wa Ardhi ya kilimo
·         Uamuzi wa baraza la Madiwani uliwasilishwa kwa kamishna wa Ardhi kwa barua kumb. Na MUD/ASF/VOL/IV /35 ya tarehe 21/9/2007.
·         Wilaya iliendelea kufanya mawasiliano ya muda mrefu na ilipofika mwaka 2009, Wizara ya Ardhi iliielekeza taratibu za kisheria zifuatwe kwa kutuma notisi kwa wamiliki wa Mashamba. Utekelezaji ni kama inavyo onekana kwenye jedwali hapa chini.
Na
Jina la shamba
Mmilikli
Tarehe ya kutuma notisi
Tarehe ya majibu
Tarehe ya kutuma mapendekezo wizara ya ardhi
Ukubwa Hekta         
1.
KIBARANGA
Consolidated holding  corporation
2/6/2009
6/8/2009
6/10/2009
5,647
2.
SAGULAS
Consolidated holding  corporation
2/6/2009
6/8/2009
17/11/2009
500
3
LEWA
Consolidated holding  corporation
2/6/2009
6/8/2009
17/11/2009
3,901
4
GEIGLTZ(Azimio kilapula)
Consolidated holding  corporation
2/6/2009
6/8/2009
17/11/2009
4,902
5
KIHUHWI
Consolidated holding  corporation
2/6/2009
6/8/2009
17/11/2009
602
6
SONGA
Jeshi la wananchi
2/9/2009
14/7/2009
17/11/2009
1,000
7
KWAFUNGO
G. Chavda (Tan farms
163/2010
Haikujibiwa
7/5/2009
2,345
8
BWEMBWERA
AMC limited Arusha
2/2/2010
Imerudishwa
7/5/2010
5730

JUMLA
24,627

·         Consolidated holdings walijibu notisi ya Halmashauri  kwa barua kumb. Na. CHC/DV/1/13/288 YA tarehe 2/0/2009 wakiiomba Halmashauri isitishe zoezi la ubatilishaji kwa malezo kwamba wanatarajia kuyapima upya mashamba hayo na kwamba baada ya kupimwa watawapatia wawezekaji binafsi pamoja na wakulima wadogo wadogo. Halmashauri haikukubaliana na suala hilo kwani sehemu kubwa ya mashamba hayo imekwishavamiwa na kupandwa mazao ya kudumu na kuendelezwa kwa makazi.
·         Tarehe 2/10/2009 Halmashauri ya Wilaya ilimuandikia Kamishina wa Ardhi barua yenye kumb. Na. MUDF /44/121 kumuomba aendelee na taratibu za ufutaji wa miliki.
·         Taratibu za ufutaji zinaendelea na kwa mara ya mwisho wizara ya Ardhi iliomba kutumiwa upya baadhi ya nyaraka za mapendekezo ya ubatilishaji wa miliki za mashamba yaliyopelekewa notisi. Nyaraka zimetumwa upya kwa Kamishina wa Ardhi kwa barua kumb. Na. MUDF/44/127 ya tarehe 16/2/2012.
·         Aidha nyaraka nyingine mpya zilitumwa kwa Kamishina wa Ardhi kwa barua kumb. Na. HW/MUH/A.10/2VOL.III/5 ya tarehe  19/10/2012.
·         Kwasasa Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya inaendelea kufuatilia kwa kuwasiliana na Wizara ya ardhi.
Pamoja na kuomba kubatilisha hati miliki za ardhi kwa baadhi ya mashamba, Wilaya inaendelea kushughulikia migogoro mingine kwa kufuata taratibu nyingine.
Baadhi ya migogoro imekwisha hususani mgogoro wa shamba mkonge Zeneth, mgogoro kati ya Kijiji cha Kibaoni na Mlingano na Mgogoro wa Kijiji cha Kiwanda na Kwafungo. Kesi zingine bado zipo mahakamani, kama ifuatvyo ;
·         Migogoro ya viwanja 148 imetatuliwa kati ya migogoro 150
·         Mgogoro wa shamba 1 umetatuliwa kati ya Migogoro 14 (13 usuruhishi unaendelea).

5.6 3 Hati miliki za ardhi.
Mashamba na viwanja 844 vimepatiwa hati
Umiliki
2011
2012
2013
Hati miliki za viwanja/mashamba
486
832
844
Upimaji wa viwanja
3,232
3,577
3,582
Jumla ya Michoro 3 imeandaliwa katika maeneo ya shamba la Chatur ikiwa na viwanja 330, Kwemkabala Viwanja 317 na Sega viwanja 22. Hati miliki zitatolewa mara baada ya taratibu za ugawaji kukamilika.

5.7 SEKTA YA MALIASILI NA MISITU
5.7.1 Misitu
Wilaya ina jumla ya hekta 47,000 za misitu, kati yake ni msitu wa asili wa Amani (ANR) uliopo katika Tarafa ya Amani. Msitu huu una viumbe mbalimbali adimu duniani pamoja na uoto wa asili unaovutia wanyama kuishi.  Wanyama wanaopatikana katika Msitu huu ni pamoja na Kima weupe, Nyoka, Vinyonga, tumbili na wengineo wengi. Pia Wilaya inayo misitu mingine ya asili 9 (Kwemarimba, Mlinga, Manga, Kambai, Nilo, kwani, Tongwe, Lunguza na Derema). Wilaya inaendeleza jitihada za kuhifadhi, kulinda, kuendeleza, uboreshaji na kuvuna maliasili za misitu na Nyuki kwa manufaa ya Taifa kama inavyoelekezwa katika ibara ya 44 ya Ilani ya Chama Tawala.

5.7.2 Ufugaji wa nyuki
Shughuli za ufugaji nyuki zinafanyika katika vijiji 8 ndani ya Tarafa 2 hapa Wilayani.  Uzalishaji wa mazao ya nyuki umekuwa ukiongezeka mwaka hadi mwaka kutoka tani 2,400 za asali na 150 za nta hadi tani 4000 za asali na 200 za nta.  Msisitizo umewekwa katika matumizi ya zana bora za ufugaji nyuki ambapo jumla ya mizinga 140 imegawiwa kwa wafugaji, na mingine 100 imenunuliwa tayari kwa kugawiwa.
Hali ya uzalishaji asali na nta ni kama inavyoneshwa hapa chini :-
Uzalishaji mazao ya nyuki
Mwaka
Idadi ya Mizinga
Uzalishaji (kg)
Asali
Nta
2010/2011
300
2400
150
2011/2012
350
2900
170
2012/2013
500
4000
200
2013/2014
1473
4500 (Matarajio)
300 (matarajio)

5.7.3 Utunzaji Mazingira.
Vijiji 15 vimeanzisha hifadhi ya misitu ya asili ambapo shughuli za utunzaji wa mazingira hufanyika. Kampeni za upandaji miti na uthibiti wa moto zinafanyika kila mwaka na hali ya upandaji miti ni kama inavyoonekana katika jedwali ;
MWAKA
IDADI YA MITI ILIYOPANDWA
2010
4,800,000
2011
2,250,300
2012
2,300,120
2013
1,516,198
Doria za mara kwa mara zinafanyika katika maeneo ya misitu na ukanda wa bahari. Pia Wilaya imewaondoa wavamizi waliovamia misitu ya Kwani na Tongwe na jumla ya miti 1,516,198 ya matunda, kuni, kivuli, mbao na viungo imepandwa kwa kushirikisha wadau mbalimbali hususani shule, mashirika na watu binafsi kwa ajili ya kuendeleza hifadhi ya mazingira.
Kampeni dhidi ya athari za moto imefanyika katika vijiji 32 vilivyo karibu na misitu ili kunusuru bionuai. Wananchi wanaoishi karibu na misitu ya hifadhi wamehamasishwa kufanya shughuli za ufugaji nyuki na vipepeo kwani shughuli hizi ni rafiki kwa Mazingira. Pia elimu inaendelea kutolewa   juu ya umuhimu wa misitu na athari za uharibifu wa mazingira.

5.8 SEKTA YA VIWANDA, BIASHARA NA MASOKO
5.8.1 SEKTA YA VIWANDA
Wilaya ina jumla ya biashara ndogo na za kati 3030, kati ya hizo viwanda vidogo ni 11, Jumla ya ajira zitolewazo na sekta ya Viwanda, Biashara na masoko ni 4,963 ambayo ni sawa na 2.1%. Wilaya inafanya juhudi za kukuza sekta ya viwanda, biashara na masoko kutoka 2.1% ya sasa hadi 3% ifikapo mwaka 2015 kwa kuboresha mazingira ya uwekezaji, kujenga masoko 2 mapya na kukarabati 1 ili kuweka mazingira mazuri kwa ajili ya maendeleo endelevu ya sekta za viwanda,biashara na masoko.Hivyo kukuza pato la mtu binafsi, Halmashauri na Taifa.

5.8.2 JUKWAA LA UWEKEZAJI
Wilaya imeshiriki katika jukwaa la uwekezaji la Kanda ya Kaskazini lililofanyika Mkoani Tanga, ambapo Fursa za uwekezaji zilizopo Wilayani zilitangazwa. Wawekezaji kumi na mmoja wameonyesha nia ya kuwekeza katika sekta za kilimo, kuongeza thamani mazao ya viungo na matunda, ujenzi wa makazi na hoteli na utalii wa kiikolojia.

Wawekezaji 2 wenye nia ya kuwekeza katika kuongeza thamini ya matunda na kusindika mihogo taratibu za kuwapatia ardhi zinaendelea, na wengine wenye nia ya kuwekeza katika kilimo na ujenzi wa makazi na hoteli mazungumzo yanaendelea.


6.0 SEKTA ZA HUDUMA ZA JAMII
6.1  SEKTA YA MAJI
6.1.1 Hali ya upatikanaji wa maji Muheza Vijijini
Watu wapatao 110,679 sawa na 62.2% ya wakazi  wanaoishi Vijijini wanapata Maji safi kutokana na vyanzo mbalimbali kama ifuatavyo:-
Miradi ya maji ya bomba ya mtiririko10, Miradi ya maji ya bomba ya kusukumwa na mashine 7, Visima vifupi vyenye pampu za mikono 175, Visima virefu vyenye pampu za mikono 23.
Hali ya upatikanaji wa maji vijijini
Mwaka
2010
2011
2012
2013
Hali ya upatikanaji wa maji
55.4%
56.3%
56.3%
62.2%

Jumla ya miradi 4 ya maji mteremko (Gravity schemes) yenye thamani ya Ths. 839,642,117.00 imekamilika kupitia mradi wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RWSSP) ambapo jumla ya watu 3,649 wamenufaika na miradi hiyo, miradi 3 ambayo inakadiriwa kugharimu Tsh. 724,722,350.00 utekelezaji unaendelea na jumla ya watu 3,762 watanufaika na miradi hii ifikapo mwishoni mwa mwaka 2013/14.  

6.1.2 Huduma ya maji Muheza Mjini
Mji wa Muheza una jumla ya wakazi 30,834 kutokana na sensa ya Taifa ya watu na makazi ya Mwaka 2012, kati yao watu 3916 sawa na asilimia 12.7% ndio wanaopata maji safi.
Huduma ya Maji ya Bomba inayotolewa Muheza Mjini inatoka katika chanzo cha Maji cha Mto Mkulumuzi unaoanzia kwenye milima ya Magoroto.  Kiasi cha maji kinachozalishwa katika chanzo hiki wakati wa mvua ni wastani wa Mita za ujazo 1,425 kwa siku na mahitaji ya wakazi wa Muheza Mjini ni Mita za ujazo 4,831 kwa siku. Mradi wa Maji ya bomba Muheza Mjini umeshapitwa na wakati kwani ulijengwa Mwaka 1977 kwa kukidhi idadi ya watu wapatao 8,000. 
Hali ya upatikanaji wa maji Mjini kwa asilimia
Mwaka
2010
2011
2012
2013
Hali ya upatikanaji wa maji
17
25
20.5
12.7

6.1.3 Mkakati wa  kupunguza tatizo la Maji Muheza Mjini.
Wilaya imechukua jitihada mbali mbali ili kukabiliana na tatizo la maji Muheza mjini. Miongoni mwa jitihada hizo ni pamoja na;
·         Kuchimba kisima cha Polisi Mang’enya kinachotumia umeme jua na chenye uwezo wa kutoa lita 5,000.
·         Kuendeleza kisima cha kitisa kilichokuwa kinatumiwa na Mamlaka ya mkonge ambapo gharama ya mradi ilimekadiriwa kuwa kiasi cha Tsh.806 milioni, kiasi cha Tsh. 229 zilitengwa toka mapato ya ndani na kuanza utekelezaji wa Mradi huu.
·         Visima virefu 9 vimechimbwa na vimefanyiwa upimaji wa ubora na wingi wa maji.
·         Wilaya iko kwenye mchakato wa kununua mtambo wa kuchimbia Visima kwa gharama ya  Tshs 250,000,000/=

6.1.4 Uvunaji wa maji ya mvua
Wilaya kwa kushirikiana na  Wadau wa maendeleo wakiwemo World Vision, World Bank na wengineo imejengakwishajenga miundombinu ya uvunaji wa maji ya mvua katika  shule za msingi 11, Sekondari 5 na Zahanati 8. Aidha jumla ya miradi 6 ya programu ya maji vijijini inayoendelea kujengwa ina kipengele cha ujenzi wa miundombinu ya maji katika taasisi za kijamii.
Ili kuongeza upatikanaji wa maji Mjini na Vijijini, Wilaya inaendelea kufanya uhamasishaji wa ujenzi wa miundombinu ya uvuanaji kwa kila nyumba iliyojengwa kwa bati.
Aidha Wilaya imetekeleza jumla ya miradi kumi na mmoja  kwa mwaka 2011/12 hadi 2012/13 yenye thamani ya Ths. 2,416,503,740.00.

6.2  SEKTA YA ELIMU
Elimu ya Msingi
Wilaya ya Muheza ina jukumu la kusimamia huduma za elimu kwa wananchi wake. Huduma ya sekta ya Elimu inajumuisha usimamizi na utoaji huduma katika ngazi ya Elimu ya Awali, Elimu ya Msingi, Elimu ya watu wazima, mafunzo ya ufundi stadi, elimu maalum, utamaduni na michezo.


6.2.1 Elimu ya Awali
Wilaya ya Muheza ina jumla ya madarasa ya elimu ya awali 113 kati ya hayo madarasa 109 yapo katika shule za msingi za Serikali na madarasa 4 yapo katika shule zinazosimamiwa na mashirika yasiyo ya Kiserikali. Idadi ya wanafunzi wanaosoma katika shule hizo ni kama ifuatavyo:
MWAKA
IDADI YA SHULE ZA AWALI
IDADI YA WANAFUNZI WA AWALI MWAKA 2011 – 2013
SHULE ZA SERIKALI
SHULE ZISIZO ZA SERIKALI
SERIKALI
BINAFSI
JML
WAV
WAS
JML
WAV
WAS
JML
2011
108
3
111
2887
2890
5777
196
217
413
2012
108
4
112
3122
3053
6175
251
241
492
2013
109
4
113
3255
3186
6441
194
168
362
Hali ya mahudhurio ya wanafunzi wa awali ni 90% . Elimu hii kwa kiwango kikubwa hufanikishwa kwa kutegemea miundo na walimu wa shule za msingi
6.2.2 ELIMU YA MSINGI
Wilaya ina jumla ya shule za msingi 115 kati ya hizo shule 111 ni za Serikali na shule 4 ni za mashirika yasiyo ya Kiserikali. Aidha shule 109 za Serikali zina darasa la I-VII na shule 2 hazijafika darasa la VII. Idadi ya wanafunzi darasa la I – VII kwa shule za Serikali ni 37,654 na shule za mashirika yasiyo ya Kiserikali ni 1,110. Jumla ya wanafunzi 7,287 wameandikishwa darasa la kwanza katika shule za Serikali na wanafunzi 251 wameandikishwa katika shule zisizo za Serikali.
Jedwali lifuatalo linaonesha mchanganuo wa uandikishaji kwa Mwaka 2011 – 2013
MWAKA
UANDIKISHWAJI DARASA LA 1
IDADI YA WANAFUNZI DARASA LA I – VII
WAV
WAS
JUMLA
%
WAV
WAS
JML
2011
4,010
3,628
7,638
100
20,517
20,043
40,560
2012
3,771
3,656
7,427
100
19,672
19,650
39,322
2013
3,865
3,673
7,538
100
18,790
18,864
37,654

6.2.2.1 Hali ya upatikanaji wa vifaa vya kujifunzia na kufundishia
Hadi kufikia mwezi Desemba  mwaka 2013 uwiano wa kitabu kwa mwanafunzi ni 1:3 kutoka 1:7 mwaka 2011 na 2012. Haya ni mafanikio makubwa yaliyotokana na ongezeko la vitabu kutokana na fedha za capitation na vitabu kutoka Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi. Aidha Wilaya imenunua vitabu 5,396 kwa fedha za capitation mwaka 2012/2013 na hadi kufikia Desemba  2013 Wilaya imepokea na kusambaza vitabu 105,000 katika shule zote 111 toka wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi na fedha za rada, hivyo kufanya jumla ya vitabu 110,396 vilivyopelekwa mashuleni hadi Desemba 2013.

6.2.2.2 Hali ya walimu
Halmashauri ya Wilaya ya Muheza ina jumla ya walimu wapatao 888. Idadi ya walimu haitoshelezi kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kustaafu, kufariki na kujiendeleza.


Mahitaji ya Walimu 2011 – 2013
MWAKA
MAHITAJI
WALIOPO
UPUNGUFU
ASILIMIA (%)
2011
1014
1001
13
1.3
2012
984
971
13
1.3
2013
981
888
93
9.5
6.2.2.3 Hali ya miundombinu.
AINA
MAHITAJI
YALIYOPO
UPUNGUFU
Madawati
13,589
12,074
1,515
Nyumba za walimu
1,161
133
1,060
Madarasa
1,055
635
420
Viti
2,431
1,238
1,193
Meza
2,346
1,116
1,230
Vyoo
1,843
1,029
814
TRcs
29
4
25

6.2.2.4 Ufaulu
Mafanikio katika jitihada za kuboresha Elimu ya msingi wilayani yanajidhihirisha kwa kuangalia matokeo ya mtihani wa darasa la IV na VII mwaka 2011 – 2013.
Matokeo ya Darasa la saba kwa kigezo cha alama 100: 2011 – 2013
Mwaka
Waliofanya
Waliofaulu
Waliochaguliwa
Wav
Was
Jml
Wav
Was
Jml
%
Wav
Was
Jml
%
Nafasi kimkoa
2011
2667
2717
5384
1789
1785
3574
66
1789
1785
3574
100
6
2012
2028
2341
4369
552
639
1191
27
1391
1681
3077
258
7
2013
2031
2181
4212
1311
1467
2778
66
1311
1467
2778
100
4

Matokeo Darasa la IV: 2011 – 2013
Mwaka
Waliofanya Mtihani
Waliofaulu Mtihani
Wav
Was
Jml
Wav
Was
Jml
%
2011
2508
2544
5052
2362
2446
4808
95
2012
2447
2523
4970
2191
2270
4461
90
2013
2379
2563
4942
2300
2523
4822
96

6.2.2.5 Matarajio ya baadae
Kuongeza asilimia ya ufaulu kwa wanafunzi wa darasa la IV kutoka asilimia 96% mwaka 2013 hadi 100% ifikapo mwaka 2014 na wanafunzi wa darasa la saba kwa kigezo cha alama 100 kutoka 66% mwaka 2013 hadi kufikia 70%  2014.

6.2.2.6 Hali ya utoro 2011 – 2013
Hali ya utoro mashuleni imepungua kwa kiasi cha asilimia 72% kutokana na juhudi zilizofanywa na Uongozi wa Wilaya.

Miongoni mwa juhudi hizo ni kuwaelimisha wazazi/walezi umuhimu wa kuwaandikisha watoto shule za jirani na makazi wanakotoka ili kupunguza umbali, kuanzisha chakula shuleni, kushirikiana na kamati za shule pamoja na kutoa elimu juu ya athari za utoro. Jedwali kuonesha hali ya utoro 2011 – 2013.
Mwaka
Wav
Was
Jml
2011
82
54
136
2012
63
52
115
2013
55
45
100

6.2.2.7 Elimu Maalumu
Wilaya ina kituo kimoja cha ulemavu wa akili katika Shule ya Msingi Masuguru chenye wanafunzi 38 kati yao Wav 24 na Was 14. Vile vile Wilaya  imeanzisha kitengo cha wanafunzi viziwi mwanzoni mwa Januari 2014 katika Shule ya Msingi Mbaramo. Hata hivyo mkakati wa mwaka 2014 ni kuendelea na kuimarisha utoaji wa Elimu Jumuishi ambapo wanafunzi wenye ulemavu wataandikishwa katika shule za kawaida za msingi wilayani.

6.2.2.8 Elimu ya watu wazima
Wilaya ina vituo vya MUKEJA vinavyoendeshwa katika maeneo mbalimbali hapa Wilayani.
Wilaya imeboresha miundombinu ikiwemo madarasa, vyoo, madawati na nyumba za walimu kwa kutekeleza miradi 11 yenye thamani ya Tsh. 149,000,000 katika mwaka wa fedha 2012/2013 hadi Januari, 2013.

Aidha Wilaya imetekeleza jumla ya miradi mitano kwa mwaka 2011/12 hadi 2012/13 yenye thamani ya Ths. 109,363,636.00.


6.2.3 ELIMU YA SEKONDARI
Wilaya ina shule za Sekondari 30, kati ya hizo 5 zinamilikiwa na watu binafsi pamoja na mashirika ya dini.

Idadi ya wanafunzi waliopo shule za Serikali kwa mwaka 2013 ni 9,099 kati yao  wavulana 4,451  na wasichana ni 4,648  wakati wanafunzi waliopo shule za Binafsi ni 1,576 wavulana ni 900 na wasichana 676. Hivyo jumla ya wanafunzi wote waliopo shule za Sekondari kwa mwaka 2013 kuwa 10,675. Aidha wanafunzi wanaotarajia kujiunga na masomo ya kidato cha kwanza kwa shule za kutwa kwa mwaka 2014 ni 2763 kati yao wavulana ni 1302  wasichana ni 1461

6.2.3.2 Usajili wa Wanafunzi Kidato cha Kwanza
Usajili kidato cha I
Mwaka
Waliochaguliwa
Walioripoti
Wasioripoti
2011
3574
3133
441
2012
3077
2232
845
2013
2778
2621
157
2014
2807
1472
1335 (hadi Januari 31)

Wanafunzi 170 sawa na asilimia 5.46% kwa mwaka 2012 wamejiunga na shule binafsi ndani na nje ya wilaya ya Muheza na wengine kubadilishiwa shule nje ya wilaya ya Muheza.
Asilimia 6.36% ya wanafunzi waliotakiwa kujiunga kidato cha Kwanza sawa na wanafunzi 198 hawakuripoti shuleni kwa sababu mbalimbali pamoja na jitihadi za kuwatafuta kutofanikiwa. Kwa mwaka 2014 bado usajili unaendelea hadi itapofika mwezi Machi.

6.2.3.2 Hali ya walimu
Halmashauri ya Wilaya ya Muheza ina jumla ya walimu wa Sekondari wenye shahada na stashahada za ualimu wapatao  431 walioko vituoni. Idadi ya walimu  inatosheleza kwa masomo ya sanaa na lugha. Aidha wilaya inahitaji walimu 144 wa Sayansi na Hisabati, waliopo ni 69 na upungufu ni 75.
Ikama ya walimu
Mwaka
Sayansi
Sanaa
Walimu wote
Mahitaji
Waliopo
Upungufu
Mahitaji
Waliopo
Upungufu
Mahitaji
Waliopo
Upungufu
2011
100
59
41
300
216
-74
400
275
125
2012
100
64
36
300
309
+9
400
373
127
2013
144
69
75
300
362
+62
444
431
13

6.2.3.3 Hali ya miundombinu.
Aina
Mahitaji
Yaliyopo
Upungufu
Madawati
9,099
9146
 47 ziada
Nyumba za walimu
365
37
328
Madarasa
375
268
107
Vyoo
564
220
344

6.2.3.4 Hali ya vifaa vya kufundishia na kujifunzia
Hadi kufikia Desemba 2013 uwiano wa kitabu kwa mwafunzi ni 1:3 hii ni mafanikio makubwa ukilinganisha na mwaka 2012 ambapo uwiano ulikuwa 1:8.

6.2.3.5 Hali ya Utoro
Hali ya utoro shuleni imepungua kwa asilimia 70% ikilinganishwa na miaka ya nyuma ambapo wanafunzi wengi walikuwa hawamalizi kidato cha nne kwa sababu ya utoro pia wazazi wengi wameelewa umuhimu wa shule na watoto wengi wanasoma shule za jirani.
Aidha kati ya sababu kuu zinazopelekea utoro ni mimba ambapo kwa mwaka 2011 waliopata ujauzito walikuwa 57, 2012 walikuwa 33 na 2013 walikuwa 29.

6.2.3.6 Maabara za Sayansi.
Hadi sasa Halmashauri ya wilaya ina maabara 8 kwa masomo ya sayansi kati ya 75 zinazohitajika, meza za maabara (mobile laboratory) 7 na madarasa ya  sayansi 17 (Vyumba vya sayansi) kwa shule za Serikali, ujenzi wa maabara 67 katika shule zote za serikali upo katika hatua mbalimbali  kwa kutumia fedha za Serikali na nguvu za Wananchi.
·         7 hatua umaliziaji.
·         2 hatua ya Lenta.
·         5 Ujenzi wa Boma
·         8 hatua ya kumwaga jamvi.
·         16 msingi umekamilika
·         20 hatua ujenzi wa msingi
·         5 Maandalizi ya awali
·         6 utekelezaji haujaanza

Lengo ni kuhakikisha kuwa Shule zote za Serikali zinakuwa na maabara tatu kwa masomo ya sayansi hadi Novemba mwaka 2014.Wilaya imejipanga kukamilisha ujenzi huo ambapo mikakati mbalimbali imewekwa ikiwemo:-
·         Michango ya wananchi kwa kila Kijiji
·         Michango ya Watumishi kuchangia kwa ngazi za mishahara
·         Mfuko wa Jimbo shule 16 zimepata Mgao wa bati 100 kila shule

6.2.3.7 Matokeo ya mitihani ya kidato cha Pili, Nne na Sita
A: KIDATO CHA PILI KUANZIA MWAKA 2010 HADI 2013
MWAKA
WALIOFANYA
MADARAJA YA UFAULU
% YA UFAULU
A
B
C
D
F
ME
KE
JML
ME
KE
JML
ME
KE
JML
ME
KE
JML
ME
KE
JML
ME
KE
JML
2010
1400
1389
2789
0
0
0
16
6
22
167
57
224
254
191
445
976
1125
2101
25
2011
1209
1140
2349
0
0
0
7
2
9
105
48
153
276
175
451
787
981
1768
26
2012
967
987
1954
0
0
0
4
9
13
114
54
168
230
211
441
629
721
1350
32
2013
923
1231
2154
2
2
4
39
5
44
215
184
399
247
356
603
416
672
1088
49

Jumla ya watahiniwa 2,557 walifanya mitihani ya kumaliza kidato cha nne kati yao wanafunzi 474 walifaulu daraja la kwanza hadi la nne sawa na 18.53% mwaka 2012 na mwaka 2013 ni wanafunzi 775 kati ya 2138 (36.2%) ya waliofanya mtihani.

B: KIDATO CHA NNE KUANZIA MWAKA 2010 HADI 2013
MWAKA
WALIOFANYA
MADARAJA YA UFAULU
% YA UFA
ULU
DIV - I
DIV   II
DIV  III
DIV    IV
FAILED
ME
KE
JML
ME
KE
JML
ME
KE
JML
ME
KE
JML
ME
KE
JML
ME
KE
JML
2010
941
896
1837
1
0
1
11
1
12
34
2
36
299
176
475
636
756
1392
29
2011
1057
1029
2086
1
0
1
3
0
3
22
5
27
281
156
429
738
851
1589
22
2012
1298
1258
2556
1
0
1
8
2
10
37
13
50
274
146
420
819
936
1745
19
2013
1102
1029
2138
 8
 1
9
 32
 17
49
119 
 54
173
 301
 244
544
 35
 713
1064
36


Wanafunzi 56 wamechaguliwa kujiunga na masomo ya kidato cha tano sawa na 11.81% ya wanafunzi waliofaulu Mtihani kwa mwaka 2013.
Aidha wanafunzi 129 walifanya mtihani wa kumaliza kidato cha sita kati yao wanafunzi 111 sawa na 86% walipata daraja la kwanza hadi la nne na wanafunzi 85 wanatarajiwa kujiunga na Vyuo Vikuu .
C: KIDATO CHA SITA KUANZIA MWAKA 2010 HADI 2013
MWAKA
WALIOFANYA
MADARAJA YA UFAULU
% YA UFAULU
DIV - I
DIV   II
DIV  III
DIV    IV
FAILED
ME
KE
JML
ME
KE
JML
ME
KE
JML
ME
KE
JML
ME
KE
JML
ME
KE
JML
2010
30
12
42
0
0
0
0
1
1
9
6
15
13
3
16
8
2
10
76
2011
37
39
76
1
0
1
7
2
9
20
20
40
6
12
18
6
2
8
89
2012
46
48
94
0
0
0
5
0
5
20
15
35
13
19
32
8
14
22
77
2013
85
43
128
1
1
2
6
2
8
53
22
75
16
10
26
9
9
18
86
























Katika kuboresha elimu hapa Wilayani miradi 10 yenye thamani ya Tsh. 721,687,326.00 imetekelezwa kwa kipindi cha mwaka 2011/12 hadi 2012/13.
6.2.4  Vyuo vya ufundi na elimu ya juu
Katika wilaya ya Muheza kuna chuo cha mafunzo ya udereva (Muheza Driving school) na chuo cha Maendeleo ya Wananchi (FDC) – Kiwanda kilichopo katika tarafa ya Bwembwera. 
Pia kuna vyuo vingine viwili vya ufundi stadi katika shule 2 za Msingi ambazo ni Mkuzi na Magila. Vituo hivi vinatoa kozi za useremala, uashi na sayansi kimu ambapo wanafunzi wanaohitimu wanakuwa na ujuzi katika fani husika.
Aidha Wilaya imetekeleza jumla ya miradi kumi na sita kwa mwaka 2011/12 hadi 2012/13 yenye thamani ya Ths.821,895,150.00.

6.3  SEKTA YA AFYA NA USTAWI WA JAMII
Wilaya ina jumla ya vituo vya kutolea Huduma za Afya 47 ikiwemo Hospitali 1 Teule. Vituo vya Afya 6 na Zahanati 41. Vituo vya Afya 4 ni vya Serikali, kituo kimoja cha Afya kinamilikiwa na Kanisa Katoliki na kimoja kinamilikiwa na Kampuni ya chai (EUTCO).
Zahanati 29 ni za Serikali na nyingine 12 zinamilikiwa na watu binafsi. Vilevile Wilaya  ina  Chuo cha Utafiti wa magonjwa ya binadamu na Taasisi ya Utafiti wa Malaria (NIMR).
Idadi ya Vituo Vya kutolea Huduma za Afya na Umiliki

Kituo cha huduma

Idadi
Mmiliki
Serikali
Kanisa
Binafsi
Hospitali
1
0
1
0
Vituo vya Afya
3
1
1
1
Zahanati
44
31
1
10
JUMLA
48
32
3
11

6.3.1 Hali ya upatikanaji wa dawa katika vituo vya Serikali:
Hali ya upatikanaji wa dawa katika vituo vya kutolea huduma ya Afya vya Serikali Wilayani Muheza ni nzuri. 
Vituo vyote vya kutolea huduma za Afya hupokea dawa kupitia vyanzo vikuu vinne navyo ni Kupitia mgao wa Wizara kwenda MSD, Mfuko wa pamoja wa Afya (HBF), Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF) na Vertical progranne kwa dawa kama ALU, Septrine na nyinginezo.
Katika kupambana na upungufu wa dawa za ILS Wilaya inaeendelea kuhamasisha Waganga Wafawidhi wa vituo vya kutolea huduma kuomba na kununua dawa kupitia fedha za CHF walizokusanya. Wilaya ya Muheza inaendelea kununua dawa kupitia Mfuko wa Basket Fund na kuzisambaza katika Vituo 33 vya kutolea huduma vya serikali.
Vituo Binafsi na vya Mashirika vimeendelea kupata mahitaji muhimu kutoka Wilayani  kama vile dawa za malaria (ALU), dawa za chanjo, dawa za TB na Ukoma, na dawa za ARV kwa wanaoishi na virusi vya UKIMWI.

6.3.2  Magonjwa ya milipuko
Kwa kipindi cha  mwaka 2010 – 2011 Wilaya ilipata   mlipuko wa ugonjwa wa Rotavirus mwezi Aprili hadi Juni 2012 ambapo watoto 325 chini ya miaka mitano waliugua na watoto saba walipoteza maisha. Pia ulijitokeza mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu ambapo watu 47 waliugua na 1 kupoteza maisha.
Mwaka 2012/2013 mwezi Machi ulijitokeza milipuko wa ugonjwa wa kuharisha uliotokana na uchafuzi wa vyanzo vya Maji ambapo jumla ya wagonjwa 180 waliambukizwa  na hakuna kifo kilichotokea.

6.3.3 Afya ya mama na Mtoto
Katika kupunguza vifo vya akina mama wajawazito kutoka vifo 375/100,000 kwa vizazi hai hadi 250/100,000, Wilaya imefanikiwa kupunguza vifo vya akina mama wajawazito kutoka 281/100,000 mwaka 2010/2011 hadi vifo 232/100,000 kwa mwaka  2012/2013. Hii ni kutokana na utoaji wa   huduma za Afya  bure  kwa  akina mama wajawazito na  watoto chini ya miaka mitano. Pia Hati punguzo 2,254 zimetolewa kwa akina mama wajawazito na watoto chini ya miaka mitano kwa ajili ya kuwakinga na ugonjwa wa malaria.
6.3.3.1 Vifo vya akinamama wajawazito:
S/NO
MWAKA
VIFO VYA AKINA MAMA WAJAWAZITO
1.
2010/2011
281/100,000
2.
2011/2012
243/100,000
3.
2012/2013
232/100,000
6.3.3.2 Chanjo
Katika kipindi cha mwaka 2010/2011hadi 2012/2013, Idara imeendelea kutoa chanjo  kwa watoto na akina mama wajawazito katika Vituo vya kutolea huduma ya Afya pamoja na chanjo mkoba vijijini.

Mchanganuo wa Chanjo  zilizotolewa kwa watoto na akina mama wajawazito  ni kama ifuatavyo:-
Aina ya chanjo
Chanjo

2010/11
2011/12
2012/13

Lengo 8,240
Lengo 8683
 Lengo 8293
BCG (Kifua Kikuu)
8,022 (97.3%)
8,188 (94.3%)
8,042 (97%)
DTPhb=Pentavalent
7984 (96.9%)
8,010 (92.2%)
7,988 (96.3%)
POLIO Kupooza
7891 (95.7%)
8,010 (92.2%)
7,992 (96.3%)
Measles (Surua)
7,818 (95%)
7,855 (90.4%)
7,946 (96%)
TT+2 (Pepopunda)
8,018 (97.3%)
8,188 (94.3%)
7,904 (95.3 %)
PCV-13(Nimonia/Kichomi
-
-
7,973 (96.1%)
Rotavirus
-
-
7,962 (96%)

6.3.4 Mfuko wa Afya ya Jamii – CHF
Wilaya ya Muheza inaendelea kutekeleza sera ya Mfuko wa Afya ya Jamii. Wilaya inafanya uhamasishaji kwa jamii, Vikundi vya Ushirika, Viongozi wa Dini, watu maarufu na wadau kujiunga na mfuko wa Afya ya Jamii (CHF). Idadi ya kaya wanachama wa mfuko zimeogezeka kutoka 1,011 mwaka 2011 hadi  kaya 7,730 mwaka 2013 sawa na ongezeko la 76% kama inavyoonekana katika jedwali;
Idadi ya kaya zilizojiunga na CHF
Mwaka
Kaya
2011
1,011
2012
1,860
2013
7,730

Kuwezesha wazee wasio na uwezo kujiunga na CHF:
  Jumla ya wazee 4,678 kati ya wazee 4617 waliolengwa wamepigwa picha kwa ajili ya kuandaliwa vitambulisho ili wawe wanachama wa mfuko wa afya ya jamii (CHF) hivyo kuwawezesha kupata matibabu katika vituo vyote 42 vya Serikali Wilayani.Vitambulisho 2099 vimeandaliwa na kufikishwa kwa walengwa

6.3.5 VVU na UKIMWI
Hali ya maambukizi ya VVU/UKIMWI imepungua kutoka 4% mwaka 2010 hadi  2.8 % mwaka 2012 kama inavyoonekana hapa chini;
Hali ya maambukizi ya VVU/UKIMWI
Mwaka
Waliopima
Kiwango cha maambukizi

Ke
Me
Jml

2010
9,456
5,668
15,124
4.0%
2011
8,242
7,122
15,364
3.0%
2012
4,632
4,040
8,672
2.8%
Pamoja na Upimaji wa VVU pia Wilaya ikishirikiana na shirika lisilo la Kiserikali la Kimarekani (LEAD PROJECT) wanatoa huduma ya Dawa za kupunguza makali ya VVU katika vituo vinne.

Aidha Wilaya imetekeleza jumla ya miradi kumi na na miwili kwa mwaka 2011/12 hadi 2012/13 yenye thamani ya Ths. 836,607,429.00.

7.0 KUENDELEZA MAKUNDI MBALIMBALI
7.1 MAENDELEO YA WANAWAKE
Ibara ya 203 ya Chama Tawala inasisitiza juu ya uendelezaji wa watoto, wakati  Ibara 204  inasisitiza juu ya kuwahusisha wanawake katika siasa, uongozi na modenaizesheni ya uchumi wetu kuwa na jamii iliyobora. Kwa kuzingatia hilo Wilaya imefanya yafuatayo ;
·         Elimu ya jinsia, ujasiriamali na uongozi imetolewa kwa washiriki 509 katika Tarafa zote 4, Lengo ni kuhakikisha kuwa wanawake wanajengewa uwezo wa kiuchumi na demokrasia ili waweze kuteuliwa na kuchaguliwa katika ngazi mbalimbali za uongozi na kuongeza nafasi za uwakilishi wa wanawake kwa lengo la kufikia asilimia 50.
·         Wilaya imetoa Mikopo jumla ya Tsh. 27,880,000 kwa ajili ya kuwakopesha vikundi 38 vya uzalishaji mali vya wanawake Wilayani. Kati ya fedha hizo kiasi cha Tsh. 8,000,000 zilitolewa na Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto.. Aidha kwa Kipindi cha mwaka wa fedha 2013/2014 kiasi cha Tsh.70,829,000 kimeidhinishwa kwa ajili ya mfuko wa wanawake na Vijana, mikopo imetolewa Tshs 35,414,500 kwa vikundi 66 vya wanawake. Wilaya inaendelea kutoa elimu ya namna ya kutumia mikopo ili kuboresha maisha ya wananchi wake.
7.7.1 Mikopo kupitia Mfuko wa Wanawake
Mwaka
Idadi ya vikundi
Idadi ya wanachama
Kiasi cha Mkopo
2010/11
38
190
8,380,000
2011/12
32
16
8,000,000
2012/13
14
70
3,800,000
2013/14
66
330
35,114,500

7.2  MAENDELEO YA VIJANA.
Wilaya ina jumla ya vijana 68,267 wenye umri kati ya miaka 15 hadi 35. Zaidi ya 70% ya vijana wameajiriwa katika sekta binafsi. Hali ya ajira kwa vijana sio nzuri kwani ajira kuu kwa wananchi wa Wilaya hii ni kilimo, wakati mazingira ya uendeshaji kilimo bado hayajakuwa rafiki kwa vijana. Hata hivyo sehemu kubwa ya vijana wamejiajiri katika bodaboda, viwanda vidogo na biashara ndogondogo.
Katika harakati za kuendeleza vijana, SACCOs ya vijana imeundwa na imesajiliwa kwa usajili namba TAR 584 ikiwa na vikundi 70 vyenye wanachama 370. Maombi ya mkopo wa Tsh. 286,300,000/= kwa ajili ya vikundi vya vijana yamewasilishwa. Wizara ya habari Michezo, Utamaduni na vijana bado unaendelea Pia Wilaya imetoa jumla ya Tsh. 49,114,000/=kwa vikundi 96 kwa mchanganuo ufuatao:
7.2.1Mikopo ya Vijana
Mwaka
Idadi ya vikundi
Idadi ya wanachama
Kiasi cha Mkopo
2010/11
16
85
6,700,000
2011/12
0
0
0
2012/13
14
70
7,000,000
2013/14
66
330
35,114,500

Juhudi zaidi zinafanyika ili kuwawezesha vijana kujiajiri na kujiongezea kipato ikiwa ni pamoja na;
·         Eneo la ekari 100 limetengwa kijiji cha Mtiti  kwa shughuli za kilimo kwa vijana.
·         Vijana 33 wametengewa maeneo katika Skimu ya umwagiliaji ya Mashewa.
·         Vijana 75 wametengewa maeneo katika Skimu ya umwagiliaji ya Misozwe.
·         Eneo la ekari 100 limetengwa kijiji  cha Mto wa Mbuzi kwa ajili ya kambi ya vijana na vijana 15 tayari wapo kambini.
·         Eneo la ekari 60 limetengwa katika kijiji cha Kwemhosi kwa ajili ya shughuli za vijana.

8.0 USAMBAZAJI UMEME
Wilaya ya Muheza ni miongoni mwa Wilaya zinazopata umeme kutoka grid ya Taifa. Vitongoji 385 kati ya 522 vilivyoko Wilayani havijapata nishati ya umeme. Idadi ya vijiji vyenye umeme imeongezeka kutoka 30 mwaka 2010 hadi kufikia 60 mwaka 2013. Mradi wa usambazaji umeme kwa ufadhili wa Serikali ya Marekani iliyoitwa Changamoto ya Millenia  (MCC – Project) umetekelezwa hapa Wilayani ambapo vijiji 14 viliungiwa umeme au kuboreshwa kwa vile vilivyokuwa tayari vina umeme, kupitia mpango huo wateja zaidi ya 40 wameunganishiwa umeme.
8.1 Ongezeko la wananchi walioungiwa umeme
Mwaka
2010
2011
2012
2013
2014 (hadi Februari)
Idadi
4348
4662
4972
5700
6100
Ongezeko

314
310
728
400

8.2 Usambazaji Umeme kupitia REA
Jitihada za kusambaza umeme katika vijiji vingine zinaendelea, ambapo Serikali kupitia wakala wa umeme vijijini REA imetoa fedha za mradi wa kusambaza umeme katika vijiji 30 hatua za awali zimeshaanza kufanyika ikiwa ni pamoja na wakandarasi kutembelea vijiji hivyo kufanya tathmini. hata hivyo upatikanaji wa umeme sio wa kiwango cha kuridhisha sana kutokana na chakavu wa miundombinu na mingine kuzidiwa na uwezo hasa baada ya kuongezeka kwa watumiaji.

8.2 Nishati mbadala
Aidha Wilaya kupitia shirika la TaTeDo inasisitiza matumizi ya nishati mbadala ambapo nishati ya umeme jua inatumika kwa kiwango kikubwa hasa katika taasisi kama shule na vituo vya kutolea huduma za Afya , kati ya mwaka 2011 hadi 2013 taasisi 15 zimewekewa umeme mbadala  ikiwemo sola 12, majiko sanifu 2 na biogas 1)

9.0 HALI YA ULINZI NA USALAMA
Hali ya ya usalama wilayani  ni ya kuridhisha, hakuna matukio makubwa yaliyotokea ambayo yanahatarisha hali ya utulivu na amani, isipokuwa makosa ya kawaida ya jinai, madai na usalama barabarani.

9.1 Mapambano dhidi ya Rushwa
9.1.1 Uchunguzi na mashitaka
Kwa kipindi cha mwaka 2010 hadi 2014 jumla ya malalamiko 153 yalifanyiwa kazi. Idara zilizolalamikiwa zaidi ni Mahakama, Polisi, Ardhi Mabaraza ya ardhi, Afya, Maji, Misitu, Utawala, Fedha, Ukaguzi, Ujenzi, Kilimo, Elimu, TANESCO, Vyama vya siasa na Benki ya NMB.

Mafanikio yaliyopatikana kutokana na chunguzi dhidi ya malalamiko haya ni kama ifauatavyo;-
·         Chunguzi dhidi ya tuhuma za vunaji haramu wa mazao ya misitu zimewezesha udhibiti wa hujuma za mapato na kuokoa jumla ya Tsh. 8,453,000/=
·         Chunguzi dhidi ya ukiukwaji wa madili ya kazi, taratibu na sheria zimewezesha hatua za kinidhamu kuchukuliwa kwa watumishi 2 wa Halmasahauri (W), migogoro 2 ya ardhi kupatiwa ufumbuzi.
·         Chunguzi katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo zimewezesha majadala 4 ya uchunguzi kufunguliwa na chunguzi zake bado zinaendelea.
·         Chunguzi dhidi ya malalamiko mengine zimewezesha kesi 4 kufunguliwa mahakamani na 2 kati ya hizo kuweza kushinda.

9.1.2 Elimu kwa Umma
Elimu juu ya rushwa, madhara yake na mustakabali wa maendeleo ya Taifa kwa ujumla imetolewa kwa jamii, miongoni mwa makundi yaliyopewa elimu ni pamoja na wananchi wa kawaida, asasi za kiraia, wanafunzi, vijana, wazee, wasanii na watumishi wa umma katika idara za Elimu, Polisi, ardhi na Serikali za Vijiji.
·         Semina 63 zimetolewa kwa jamii
·         Mikutano ya hadhara 26 imefanyika kwa baadhi ya jamii
·         Mijadala ya wazi 10 imefanyika
·         Klabu 30 za wapinga rushwa zimeendelea kuimarishwa katika shule za Sekondari na vyuo.
·         Klabu 27 za wapinga rushwa zimefunguliwa katika shule za msingi.

9.3.3 Udhibiti
Jumla ya dhibiti 10 zimefanyika katika kuhakikisha sekta za umma na binafsi zinatoa huduma kwa jamii kwa kuzingatia sheria, kanuni, taratibu na mifumo inayozingatia uwazi na uwajibikaji kwa lengo la kupunguza kero na malalamiko ya wanajamii.
Aina ya dhibiti zilizofanyika ni pamoja na;
·         Udhibiti 1 wa kusitisha utekelezaji wa zabuni iliyotolewa na Halmashauri (w)
·         Vikao 2 vya udhibiti baina ya TAKUKURU na Uongozi wa Halmashauri (w)
·         Kikao 1 cha udhibiti kati ya TAKUKURU na uongozi wa baraza la Kata Mkuzi
·         Udhibiti 1 na kikao 1 cha udhibiti kati ya TAKUKURU na Jeshi la Polisi
·         Udhibiti 1 dhidi ya utoaji haki ya dhamana katika Mahakama ya Mwanzo
·         Udhibiti mmoja dhidi ya taratibu za utoaji wa mikopo katika Benki ya NMB
·         Udhibiti 1 dhidi ya taratibu za uunganishaji umeme kwa wateja wa TANESCO.
·         Kikao 1 cha udhibiti kati ya TAKUKURU na Chama Cha Walimu cha Kuweka na Kukopa (UWAKAMU)

9.2 Mapambano dhidi ya madawa ya kulevya
Kwa kipindi cha Januari 2013 hadi Februatri 2014 makosa 46 ya aina mbalimbali yamefanyika kama ifauatavyo;
·         Makosa ya kupatika na bango    - 20
·         Makosa ya kupatika na mirungi - 11
·         Makosa ya kupatika na cocaine - 1
·         Makosa ya kupatika na pombe ya moshi           - 14

Katika makosa haya jumla ya watuhumiwa 84 walikamatwa na kufikishwa mahakamani, kati ya hizo kesi 20 bado zinaendelea, kesi zilizoshinda ni 21 na zilizoshindwa 5.

Serikali ikishirikiana na Wadau wengine inaendelea kutoa elimu kwa jami juu ya atharai za kutumia madawa ya kulevya.

11.0     MAFANIKIO
Mheshimiwa Rais,
Wilaya yetu imefanikiwa katika maeneo yafuatayo; 
·         Tumeongeza Ukusanyaji wa mapato kutoka Tshs 821,525,858 mwaka 2011/2012 hadi kufikia Tsh 1,164,934,499 mwaka 2012/2013.
·         Ukusanyaji wa mapato bila ya fedha za fidia ya vyanzo vilivyofutwa kutoka Tsh 755,672,857 mwaka 2011/2012 hadi kufikia Tsh  855,646,270
·         Halmashauri imepata hati safi kwa miaka minne (4) mfululizo kutoka 2009/2010 hadi 2012/2013.
·         Vituo vya kutolea huduma za afya vimeongezeka kutoa 29 hadi vituo 33 kwa mwaka 2012/2013.
·         Kasi cha maambukizi ya VVU imepungua kutoka 3% hadi kufikia 2.8%  mwaka 2012
·         Wilaya imefanikiwa kupunguza vifo vya akina mama wajawazito kutoka 281/100,000 mwaka 2010/2011 hadi vifo 232/100,000 kwa mwaka  2012/2013
·         Ufaulu wa shule za msingi umeongezeka kutoka 29.26%  mwaka 2012 hadi 66% mwaka 2013
·         Kiwango cha upatikanaji maji safi na ya uhakika kimeongezeka toka 56.3% mwaka 2011 hadi 62.2% mwaka 2013



12.0 CHANGAMOTO
Mheshimiwa Rais,
Kumekuwa na changamoto mbalimbali zilizojitokeza
1.      Uhaba wa upatikanaji wa maji safi na salama kwa ajili ya matumizi ya majumbani hususani wakati wa kiangazi maji yanapungua sana. Hii inatokana na kuwa na chanzo cha maji cha muda mrefu kisichokuwa na uwezo wa kutosheleza mahitaji kwa idadi ya wakazi wa Muheza kwa sasa.
2.      Uharibifu wa mazingira unaofanywa na wachimbaji haramu wa madini katika misitu ya asili ya Amani, unaosababisha kuharibika kwa  vyanzo vya maji na bioanuwai.
3.      Migogoro ya ardhi inayosababishwa na eneo kubwa la wilaya kuwa ni mashamba yanayomilikiwa na makampuni au wawekezaji (Private Investors) na yale ambayo yako chini ya Consolidated Holding, mashamba haya yametelekezwa kwa muda mrefu hivyo kufanya wananchi kufanya uvamizi. Mashamba yaliyotelekezwa na wamiliki binafsi ni Bwembwera, Kwafungo, Mtindiro na mashamba mawili ya Wilaya ambayo ni Zigi Mimbeni na Chartur. Mashamba yaliyopo chini ya Consolodated Holding ni Kibaranga linalosimamiwa na Bodi ya mkonge Tanzania, Geiglitz (Azimio/ Kilapura), Lewa, Sagulas na Mivumoni.
4.      Umasikini wa kipato kisichotosheleza
5.      Hali ya barabara yetu itokayo Muheza kuelekea Tarafa ya Amani haiko katika hali nzuri. Barabara ya Muheza hadi Amani ipo chini ya uangalizi wa TANROAD.
6.      Upungufu wa watumishi husuani katika kada za Afya, walimu, Kilimo na watendaji wa Vijiji. Wilaya ina upungufu wa watumishi 242.

13.0 UFUMBUZI WA CHANGAMOTO
1.      Kutekeleza mpango wa muda mrefu wa kutoa maji ya mtiririko kutoka mto Zigi umbali wa kilometa 22 hadi Muheza mjini mara baada ya kupata fedha toka Serikali Kuu.  Upembuzi yakinifu umekwishafanyika, mchoro na makisio ambayo yanafikia shilingi bilioni 13.4 yamekwishafanyika na kuwasilishwa Wizara ya Maji, na kwakuwa hii ilikuwa ndiyo ahadi yako Mheshimiwa Rais, uliyoitoa kwa wakazi wa wilaya ya Muheza wakati wa Kampeni za Uchaguzi mwaka 2010, tuna matumaini kuwa mradi huu utafanikiwa.
2.      Wilaya imeanza kutatua tatizo la upungufu wa maji Muheza mjini kwa kuanzisha miradi ya muda mfupi. Miradi hiyo ni ujenzi wa kisima kirefu Polisi Mang’enya ambao umekamilika,  kununua mashine ya kuchimbia visima ambayo taratibu za manunuzi zinaendelea na kuchimba visima 10 ambapo visima 9 vimeshachimbwa, kazi iliyobaki ni kuweka pampu ili maji yasukumwe kuingia katika mtandao wa maji uliopo.
3.      Mradi wa shughuli za kiuchumi katika eneo la hifadhi hai ya Amani umeanzishwa kupunguza utegemezi  katika mazao ya misitu
4.      Mkakati wa upandaji miti umewekwa kwa kila shule kuwa na kitalu cha miche 4000.
5.      Mkoa pamoja na Wilaya imepiga marufuku uvunaji wa misitu
6.      Usimamizi na doria ya mara kwa mara umeimarishwa.
7.      Wilaya imependekeza Serikalini mashamba kumi yabatilishwe miliki zake na kukabidhiwa kwa Halmashauri ili yaweze kugawiwa kwa wananchi wenye shida ya ardhi. Mashamba yaliyoombewa kubatilishwa miliki ni Sagulas, Lewa, Geiglitz (Azimio/ Kilapura), Kihuhwi, Songa ambalo limependekezwa kumegwa, Kwafungo, Bombwera, Mivumoni, Zeneth, Kibaranga na Chartur.
8.      Wilaya inaendelea kutekeleza miradi mbalimbali inayolenga kuongeza kipato cha mwananchi mmojammoja , na hasa kuweka msisistizo katika kuboresha mazao ya biashara ya Machungwa na viungo.
9.      Wilaya imeendelea kuboresha barabara ya Amani – Muheza kadri fedha zinavyopatina, pia kuwakumbusha Wakala wa barabara TANROAD kila mara ili kuweaka katika mipango yake.
10.  Maombi ya ajira mpya yamepelekwa Sekretarieti ya ajira kwa ajili ya kuwapata watumishi.

14.0 HITIMISHO
Mheshimiwa Rais,
Tunatoa shukrani zetu za dhati kwa Serikali kwa kutupatia fedha zilizowezesha utekelezaji wa  miradi katika sekta mbalimbali  katika Wilaya yetu.
Pia tunashukuru kwa msaada ambao umekuwa ukiutoa kwa Wilaya yetu hasa katika kukabiliana na kero ya maji, migogoro ya ardhi na  shughuli za kuinua uchumi/kutuongezea kipato.
Baada ya maelezo haya, tuko tayari kupokea maagizo na maelekezo yatakayotuwesha kuboresha utendaji wetu wa kazi.

Kwa heshima kubwa naomba  kukukaribisha Wilayani Muheza.



Mhe. Subira Mgalu (MB)
MKUU WA WILAYA
MUHEZA













 Raisi wa Jamuhuri ya Muungano waTtanzania  Mhe. Dkt Raisi Jakaya Mrisho Kikwete akikagua majengo ya shule moja wapo iiliyopo wilayani ya muheza.

Raisi wa Jamuhuri ya Muungano waTtanzania  Mhe. Dkt Raisi Jakaya Mrisho Kikwete akikagua mizinga ya nyuki ikiwa ni mradi wa ufugaji wa nyuki wilaya ya muheza.














MIRADI
  ITAKAYOTEMBELEWA

NA

KUWEKEWA MAWE

YA

UZINDUZI


TAARIFA FUPI YA UJENZI WA SOKO LA MICHUNGWANI-MUHEZA KWA MHESHIMIWA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
DK. JAKAYA MRISHO KIKWETE.

UTANGULIZI:
Mradi huu ulianza baada ya kuongezeka kwa wafanyabiashara kwenye soko kuu la Muheza Mjini,  Wingi wa wafanyabiashara ulisababisha kutokuwa na nafasi ndani ya soko na kupelekea upangaji wa bidhaa chini ardhini nje ya soko kinyume na taratibu za Afya.

Hata hivyo wazo hilo limekuwa ni moja ya Utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) ya mwaka 2010 ibara ya 49 ambayo inaelekeza kuweka mazingira mazuri kwa ajili ya maendeleo endelevu ya sekta ya viwanda, biashara na masoko.

UTEKELEZAJI WA MRADI:
Mradi huu hadi kukamilika kwake utakuwa na majengo makubwa 3 ambayo ni;
§  Jengo la mbogamboga na matunda,
§  Jengo la nafaka na
§  Jengo la wauzaji wa jumla
Pia kutakuwa na vibanda vya ofisi, maduka na migahawa kuzunguka soko zima pamoja.

Ujenzi wa soko la vyakula.
Jengo la kwanza la soko limejengwa kwa awamu mbili (2) na Wakandarasi tofauti. Hatua ya kwanza ilihusisha ujenzi wa jengo lenyewe hadi kupaua na awamu hii ya mradi ilianza tarehe 21/06/2011 na ukakamilika tarehe 17/12/2011. Mkandarasi aitwae MASIA CONSTRUCTION & GENERAL SUPPLY LTD kwa mkataba Na. MUH/DC/LGCDG/10/11/02 wenye thamani ya Tsh63,021,454/= 

Awamu ya pili iliyohusisha umaliziaji wa soko na ujenzi wa vizimba ilianza tarehe 24 July, 2012 na kukamilika tarehe 24 Octoba 2012, Mkandarasi aitwae FAIR CLASS CONSTRUCTION LTD wa Morogoro kwa mkataba Na. MUH/DC/LGCDG/2011/2012/05 wenye thamani ya Tshs.49,588,700/= hivyo thamani ya mradi ni 112,607,154/=

Ujenzi wa soko la mboga mboga na matunda.
Ujenzi wa mradi huu ulianza tarehe 02/10/2013 kwa mkataba namba LGA/MDC/CTB/LGCDG/2012/2013/10  Mkandarasi aitwae COOPERATION SOLE WORKS, ujenzi kwa awamu hii umemalizika tarehe 02/03/2014 kwa mkataba wa Tsh. 102,381, 600/=.

FAIDA ZA MRADI
§  Mradi huu umetoa fursa kwa wafanyabiashara wadogo 48 kupata meza za kuuzia bidhaa, na awamu ya pili itakapokamilika utaweza kutoa ajira kwa wafanyabiashara 72. Aidha soko hili hutoa ajira kwa wafanyabiashara watao 2,000 kwa siku za magulio.
§  Mradi utasaidia  kupunguza urefu wa mwendo kwa wakazi wasiopungua 13,513 wa maeneo ya Kata ya Genge na Majengo ambao awali walikuwa wanategemea kupata mahitaji yao toka Soko Kuu la Muheza Mjini.
§  Pia mradi utasaidia kuongezea mapato kutokana na ushuru.

MIPANGO YA BAADAYE
§  Ujenzi wa jengo la kuchambua, kufungashia na kuhifadhia matunda, mradi huu unatarajiwa kuanza mara taratibu za manunuzi zitakapokamilika,.  Mradi unategewa kuongeza thamani ya matunda yanayozalishwa Wilayani kwa kuchambua kwa madaraja, kufungasha na kuhifadhi katika vyumba vya baridi. Tayari Wilaya imetenga kiasi cha Tsh. 74 milioni.
§  Kujenga vibanda vitakavyozunguka soko ikihusisha eneo la kupaki magari na maduka ya nyama. Kazi hii inatarajiwa kufanywa kwa ubia (PPP). Ujenzi wa vibanda na maduka utakapokamilika pia utaongeza wigo wa ajira na kipato kwa wakazi wa Muheza.
§  Kuendelea kutenga fedha za kutosha kwenye bajeti ya mwaka 2014/2015 kwa ajili ya uboreshaji wa miundombinu ya soko ikiwemo vyoo, maji na barabara
§  Taratibu za kuomba mkopo toka taasisi za fedha na ushirikiano wa wadau binafsi (PPP) kwa ajili ya ujenzi wa soko la samaki.

HITIMISHO
Mhe. Rais,
Tunaishukuru Serikali kutupa fedha zilizowezesha utekelezaji wa mradi huu wa soko ambao unatoa huduma kwa wananchi wa Muheza. Pia tunakushukuru wewe binafsi kwa kuja kututembelea na kukagua shughuli zetu za maendeleo ikiwemo mradi huu.
Mwisho tunakuomba utufungulie mradi wetu.





KARIBU SANA.










TAARIFA FUPI YA SHULE YA SEKONDARI POTWE- MUHEZA   KWA MHESHIMIWA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
DK. JAKAYA MRISHO KIKWETE.
1.   Utangulizi
 Mheshimiwa  Rais
Kwa niaba ya viongozi na wanafunzi  wa shule hii ninatanguliza shukrani zetu za dhati kwa kukubali kutenga muda wako na kuja kututembelea haswa katika shughuli hii maalumu ya ukaguzi wa ukarabati wa madarasa sita, ujenzi wa maabara ya sayansi, ujenzi wa vyoo matndu 8 na umaliziaji wa nyumba ya mwalimu.
         Tunayofuraha kubwa kukukaribisha hapa Shuleni kwetu.

2.   Historia ya Shule
Shule ya Sekondari Potwe  ipo katika kitongoji cha Kiwanjani katika kijiji cha Potwe Mpirani kata ya Potwe, tarafa ya Bwembwera umbali wa kilomita 30 toka makao makuu ya Wilaya na Kilomita 8 toka barabara kuu itokayo Tanga kwenda Segera. Shule ina eneo la ekari 38.9.

Shule hii ni ya kutwa na mchanganyiko na ina kidato cha kwanza hadi cha nne  (I- IV). Shule ilianzishwa mwaka 2006 ikiwa na vyumba viwili (2) vya madarasa na jumla ya wanafunzi 59,  waalimu watatu na wafanyakazi wengine wawili. Shule ilipata usajili wa namba S.2012 na kituo cha mtihani wa Baraza S.2255. Kwa sasa shule ina idadi ya vyumba kumi (10) vya madarasa na ofisi tatu. Idadi ya wanafunzi ni 249 kati yao wavulana ni 129 na wasichana 120, ikiwa na waalimu 19 (wanaume 14 na wanawake 5) ambao wamepangiwa mnamo mwaka 2013 baada ya kuwa na upungufu kwa muda mrefu.  Shule inafanya mitihani ya Mock na Taifa kwa kidato cha pili na cha nne na matokeo ni ya wastani.

3.   UTEKELEZAJI WA MRADI.
          Ujenzi ulianza rasmi tarehe 30/07/2013 ukihusisha ujenzi  wa maabara moja itakayo tumika katika masomo matatu yaani  Fizikia, Baiolojia na Kemia, ujenzi wa choo cha wanafunzi matundu nane (8). Ukarabati wa madarasa sita na ofisi mbili za walimu na umaliziaji wa nyumba moja ya mkuu wa shule, kazi hii imefanywa na Mkandarasi wa kampuni ya Kimataifa ya MOTOSACHI  ya Dar es salaamu, iliyo ingia mkataba namba LGA / MUH/DC/ED 2012/2013/02. Wenye thamani ya Tsh. 217,509,800.




4.   Faida za mradi.
          Mradi huu umekuwa na manufaa kishule, kijamii na kitaifa kwa ujumla, ikiwemo;
·         Wanafunzi watapata fursa ya kujifunza masomo ya sayansi kwa vitendo ambayo huwa ni vigumu kueleweka bila mafunzo kwa vitendo. 
§  Ongezeko la ufaulu kwa masomo ya sayansi kutaipa shule fursa ya kutoa watalamu wa sayansi katika Taifa .

Hakika  mradi umepokelewa kwa furaha  kama mkombozi kwa wanajamii, pia kwa sasa tunaendelea na ujenzi wa maabara zingine mbili kwa nguvu za wanakijiji  hadi sasa mradi huo umefika hatua ya jamvi.

5.   Changamoto
         Changamoto zinazo ikabili shule ni pamoja na:-
§  Uhaba wa nyumba za walimu, kwani kuna nyumba mbili pekee za waalimu
§  Ukosefu wa umeme na maji suala linalowapelekea wanafunzi kutafuta huduma ya maji umbali mrefu.
§  Upungufu wa walimu wa Sayansi ambapo wapo watatu na mwalimu wa hisabati hakuna kabisa.
§  Ukosefu wa mabweni ya wanafunzi hasa ikizingatiwa kuwa wanafunzi wengi wanatoka vijiji vya mbali.
§  Ukosefu wa jengo la utawala , Bwalo la chakula na jiko.

6.   Mikakati ya kukabiliana na changamoto.
·         Halmashauri kuendelea kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa miuondombinu ya shule pia kuhamasisha wananchi kuchangia katika shughuli za ujenzi wa miundombinu.
·         Halmashauri kwa kushirikiana na mashirika yasiyo ya kiserikali kama World Vision kuomba kusogeza huduma ya maji katika maeneo ya shule na vijiji vya jirani.
·         Kuendelea kupanga waalimu wa sayansi kulingana na mgao wa waalimu kwa mwezi March, 2014 kutoka Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi.

MWISHO
Tunaishukuru Serikali kutupa fedha zilizowezesha utekelezaji wa mradi huu wa ukamilishaji wa miundombinu ya shule. Pia tunakushukuru wewe binafsi kwa kuja kututembelea.

Kwa heshima tunaomba ukague shughuli zilizofanywa katika uboreshaji wa miundombinu ya shule yetu.



KARIBU SANA.


TAARIFA YA MRADI WA MAJI KATIKA KIJIJI CHA KWEMHOSI - MUHEZA KWA MHESHIMIWA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
DK. JAKAYA MRISHO KIKWETE.

UTANGULIZI.
Katika kutekeleza Ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010- 2015 ibara ya 86 Halmashauri ya Wilaya  ya Muheza imetekeleza mradi wa maji katika kijiji cha Kwemhosi ili kupunguza kero ya maji kwa wananchi wa kijiji hicho.

UTEKELEZAJI WA MRADI
Kijiji cha Kwemhosi ni moja kati ya vijiji kumi vilivyochaguliwa na Halmashauri ya Wilaya Muheza ili kutekeleza mradi wa Maji kupitia Mpango wa WSDP (Water Sector Development Program).

Mradi wa Maji Katika Kijiji cha Kwemhosi umejengwa na Mkandarasi aitwaye SERICO COMPANY LTD ya Dar Es Salaam akisimamiwa na Kampuni ya Ushauri ya COWI TANZANIA kwa mkataba Na. LGA/MUH//WSD/2012/2013/01. Mradi huu ulikuwa wa kipindi cha Miezi sita kuanzia tarehe 28 February, 2013 hadi tarehe 28 August, 2013.

Gharama za Mradi huu hadi kukamilika kwake ni kiasi cha Tsh. 224,996,000.00
Kazi zilizofanyika katika mradi huu ni kama ifuatavyo:-
1.    Kujenga tank la lita 90,000
2.    Kujenga fence kuzunguka eneo la tank
3.    Kujenga vituo 12 vya kuchotea maji
4.    Kuchimba mtaro na kulaza bomba kiasi cha kilometa 7.17
5.    Kujenga Manhole chemba 30
6.    Kuweka alama 25 sehemu zilipopita bomba (Markers)

Kabla ya mradi huu wakazi wa kijiji hiki walikuwa wanapata maji kutoka katika kisima kirefu kilichochimbwa na Halmashauri kupitia program ya Maji Vijijini na walikuwa wanatembea umbali wa kilometa 1 kufuata huduma ya maji.
Mradi huu hadi kukamilika una uwezo wa kutoa lita 90,000 za maji kwa siku na unahudumia jumla ya wakazi 1,604  kutoka katika kijiji cha Kwemhosi.

HITIMISHO
Tunaishukuru Serikali kutupatia fedha zilizowezesha utekelezaji wa mradi huu wa  maji ambao unatoa huduma kwa wananchi wa kijiji cha Kwemhosi. Pia tunakushukuru wewe binafsi kwa kuja kututembelea na kukagua shughuli zetu za maendeleo ikiwemo mradi huu.

Mwisho tunakuomba utuzindulie mradi wetu.


KARIBU SANA

TAARIFA YA UNUNUZI WA MTAMBO WA KUCHIMBA VISIMA VIREFU - MUHEZA KWA MHESHIMIWA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA DK. JAKAYA MRISHO KIKWETE.

1.   UTANGULIZI:
Mheshimiwa Rais.
Katika kutekeleza Ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010 -2015 ibara ya 86 inaelekeza  kuongeza upatikanji wa huduma ya maji salama kufikia asilimia 65 vijijini na mijini asilimia 75 ifikapo mwaka 2015. Wilaya ya Muheza imejipanga vizuri kukabiliana na tatizo la maji lililopo Muheza.

Uongozi wa Wilaya kupitia Baraza la Madiwani la Halmashauri liliazimia kununua mashine ya  kuchimbia visima vya maji kwa kutumia fedha zake za mapato ya ndani. Mtambo huo unafahamika kwa jina la PAT – DRILL 401 AND COMPRESSOR ATLAS COPCO XAHS 186] wenye uwezo wa kuchimba visima virefu hadi kufikia mita 150 – 200 kwa kiasi kidogo cha dizeli (40) na kupasua miamba.

1.   UTEKELEZAJI WA MRADI
Mchakato wa ununuzi wa mashine ya kuchimba visima virefu (PAT – DRILL 401 AND COMPRESSOR ATLAS COPCO XAHS 186] ulianza tarehe 04.06.2013  ambapo Halmashauri ilifanya mawasiliano na PAT – DRILL 401 AND COMPRESSOR ATLAS COPCO XAHS 186 iliyopo Nairobi Kenya. Baada ya kuona gharama zake ziko juu. Wilaya iliamua kufuatilia Gharama za Ununuzi wa Mtambo huo kwa Makao Makuu ya Kampuni ya “PROMOTION OF APPROPRIATE TECHNOLOGY CO. LTD, BANGKOK, THAILAND” na kugundua kuwa gharama za ununuzi ni USD 137,835.63 sawa na Tshs 227,428,789.5 ikiwa kuna tofauti ya USD 56,541.7 sawa na Tshs 93,293,805 kwa kufanya manunuzi hayo Kenya. Gharama ya ununuzi wa mtambo kutoka Bangkok Thailand zinahusisha pia gharama za bima ya mtambo na usafirishaji wa mtambo mpaka Bandari ya Dar- Es-Salaam [CIF].

  1. MCHAKATO WA MALIPO.
Kwa minaajili ya kujihakikishia usalama wa fedha za Halmashauri, Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji iliwasiliana na Benki ya CRDB ili iweze kufanya malipo kwa niaba yake kupitia “Documentary Credit No. CRDB13ILCxxx”.
Hata hivyo, kabla ya mashine hiyo kusafirishwa na kuingia Tanzania, ilikaguliwa, yaani umefanyiwa “Pre Shipment Verification of Conformity - PVoC” ambapo Mamlaka ya Viwango Tanzania - TBS wana wakala nchini Thailand – [SGS Thailand]. Hivyo basi gharama za mtambo ni Tsh. 249,140,622.54 kama ifuatavyo; Gharama ya ununuzi wa mtambo   Tsh. 231,522,100.00, Gharama ya Ukaguzi, Bima, Ushuru wa forodha, utoaji bandarini, usafirishaji Tanga – Muheza ni Tsh. 17, 612,522.54.



    
3.   USAFIRISHAJI
Tarehe 23/01/2014 mtambo umesafirishwa kutoka Bandari ya Bangkok Thailand kuelekea Bandari ya Dar-Es-Salaam – Tanzania.
Hata hivyo baada ya kupokea “Bill of ladding“ Halmashauri iliweza kufanya mawasiliano na Wakala wa Meli iliyosafirisha Mtambo huo na kupata taarifa kwamba meli hiyo itapita bandari ya Tanga tarehe 27/02/2014 mpaka tarehe 2/03/2014 na kutuwezesha kufanya maombi ya kubadilisha Bandari ya kupokelea mtambo. Tarehe 27/02/2014 mtambo huo ulishushwa bandari ya Tanga.  

4.   FAIDA ZA MRADI.
·         Kuongeza na kuboresha huduma ya upatikanaji maji katika Wilaya
·         kupunguza  gharama za uchimbaji wa visima hapa Wilayani.
·         Kuongeza wigo wa ajira kwa wakazi wa Muheza
·         Kuongeza mapato ya Halmashauri kutokana na kazi ya kuchimbia visima endapo mtambo utakodishwa.   

5.   MIPANGO YA BAADAYE
Hili kuhakikisha Matumizi ya Mtambo huu yanakuwa endelevu , Halmashauri ya Wilaya Muheza imepanga kufanya yafuatayo:
·         Kutoa mafunzo kwa wataalam wa Halmashauri ambapo Mtaalam kutoka Kampuni ya Pat-drill Kenya atatoa mafunzo.
·         Kutunga sheria ndogo za uendeshaji wa mtambo ambapo Kijiji/Eneo lolote kitakalochimbwa kisima wananchi watachangia kiwango kitakachopitishwa na Halmashauri ili Mtambo huu uweze kujiendesha wenyewe.
·         Kuunda Kamati ya uendeshaji

MWISHO
Tunakushukuru kwa kuja kututembelea na kukagua miradi ya maendeleo. Kwa heshima tunaomba ukabidhi mtambo wa kuchimba visima viongozi wa Wilaya.








KARIBU SANA










TAARIFA FUPI YA UFUGAJI NYUKI KWA VIJANA - MUHEZA KWA MHESHIMIWA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
DK. JAKAYA MRISHO KIKWETE.

UTANGULIZI.
Halmashauri ya Wilaya ya Muheza imeazimia kutumia fursa ya Ufugaji Nyuki kwa lengo la Kuboresha na Kuongeza Kipato kwa Vijana. Ili kutimiza azma hiyo, mkakati maalum wenye lengo la kuhamasisha, kuratibu na kusimamia shughuli hiyo umeanzishwa rasmi. Mkakati huo unafahamika kama“Mpango wa Ufugaji Nyuki kwa Vijana”ambao kwa kifupi unaitwa “MUNVI”.

MALENGO.
 Mpango wa Ufugaji Nyuki kwa Vijana unalenga kutoa hamasa kwa vijana mbalimbali waliopo katika Wilaya ya Muheza, hasa kwenye maeneo yenye fursa nzuri kwa Ufugaji wa Nyuki. Kwa kuanzia, vijana wapatao 100 watawezeshwa chini ya mpango huu ili waweze kujiajiri kupitia Sekta ya Ufugaji Nyuki katika vijiji 10, ambavyo ni Vijiji vya Kazita , IBC Msasa, Mgambo Miembeni, Kimbo, Mashewa, Sakale, Kilongo, Mto wa Mbuzi, Mlingano na Mhamba .

Mpango huu utawajengea uwezo vijana hawa kwa kuwapa Mafunzo ya Mbinu Bora na za Kisasa za Ufugaji wa Nyuki. Mpango unategemea pia kuwapa vijana vifaa muhimu kama Mizinga ya Kisasa 5000 na Mavazi ya Kinga za Nyuki jozi 500.

Vijana wataweza kuzalisha mazao ya Nyuki kama Asali na Nta, kuyauza na kujipatia Kipato. Pia kwa njia hii watakuwa wanachangia na kuhamasika kutunza Mazingira kwa kuwa Nyuki ni Baioanuai rafiki wa Mazingira. Vijiji vinasaidia kutenga maeneo kwa ajili ya vijana hawa kuweka/kutundika mizinga yao.

UTEKELEZAJI
Kwa mwaka 2013/14, mpango huu umeanza utekelezaji wake katikaTarafa ya Amani ambako unafanya kazi na Umoja wa Wafugaji Nyuki Amani, “UWANA”.Umoja huu una jumla ya wanachama 45, wavulana 30 na wasichana 15. Umoja ulianza na Mizinga ipatayo 20 mnamo mwaka 2009 na kwa sasa kuna Mizinga ipatayo 133. Lengo la umoja huu ni kufikisha idadi ya Mizinga 2,000 ifikapo mwaka 2020.

Mpango wa Ufugaji Nyuki kwa Vijana unatoa Mizinga ya Kisasa 100 yenye thamani ya Tsh. 6,500,000/= kwa Umoja wa Wafugaji Nyuki Amani ili kuchangia katika juhudi zao za uzalishaji wa asali kwa lengo la kujiongezea kipato.

MAFANIKIO
Umoja huu kwa sasa unauwezo wa kuzalisha Lita 600 zaAsali kwa mwaka, na huingiza fedha kiasi cha Shilingi Milioni Nne na Laki Mbili kwa mwaka (Tshs 4,200,000/=).


CHANGAMOTO
  • Kikundi kinakabiliwa na uhaba wa vifaa na vitendea kazi muhimu kama vile:-Mizinga, Mavazi ya Kinga, Zana za Mizinga, Mitambo ya Kurinia Asali, Vifaa vya Kuhifadhi na Kufungashia Asali.
  • Kuwepo kwa wadudu waharibifu (wanasumbua nyuki)
  • Ukosefu wa Elimu juu ya ufugaji wa nyuki.

MIKAKATI YA KUKABILIANA NA CHANGAMOTO
  • Kuendelea kuwapatia vifaa na vitendea kazi muhimu kadiri uwezo utakavyoruhusu.

  • Kutoa elimu ya kupambana na wadudu waharibifu na wasumbufu kwa Nyuki ikiwa ni pamoja na kusaidia dawa za kudhibiti wadudu hao.

  • Kutoa elimu ya Ufugaji Bora wa Nyuki kwa njia ya kisasa kwa lengo la kuzalisha Asali na Mazao mengine ya Nyuki kibiashara.

HITIMISHO
Mhe Rais
Tunaishukuru Serikali kutupa fedha zilizowezesha utekelezaji wa mpango huu. Pia tunakushukuru wewe binafsi kwa kuja kututembelea na kukagua shughuli zetu za maendeleo ikiwemo kukabidhi mizinga ya kisasa 100 kwa Umoja wa wafugaji nyuki Amani.

Mwisho tunakuomba ukabidhi mizinga ya nyuki.





KARIBU SANA.






Next
This is the most recent post.
Older Post

0 comments:

Post a Comment